-
Yehova Hubariki Ibada SafiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Lakini, mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge [“mwenye kuteseka,” “NW”], mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.” (Isaya 66:2b)
-
-
Yehova Hubariki Ibada SafiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
6. Ni katika maana gani waabudu wa kweli wanapaswa ‘kutetemeka wasikiapo neno la Mungu’?
6 Kwa kuongezea, Yehova huwatafuta wale ‘watetemekao wasikiapo neno lake.’ Je, hii inamaanisha kwamba anataka tutikisike kwa hofu kila tunaposikia matamko yake? Sivyo, bali anatutaka tuyaone maneno yake kwa kicho na staha nyingi. Tunatafuta shauri lake kwa moyo mweupe, tukilitumia ili litupe mwongozo katika shughuli zote za maisha. (Zaburi 119:105) Tunaweza pia ‘kutetemeka’ katika maana ya kuhofu tusije tukakosa kumtii Mungu, kuichafua kweli yake kwa mapokeo ya kibinadamu, au kuiona kama mchezo tu. Mtazamo huo wa unyenyekevu ni muhimu katika ibada safi—lakini inahuzunisha kwamba ni watu wachache walio na mtazamo huo katika ulimwengu wa leo.
-