Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Saa Ya Hukumu” Imefika
    Endeleeni Kukesha!
    • Anasema hivi kwa sauti kubwa: “Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imefika.” (Ufunuo 14:6, 7)

  • “Saa Ya Hukumu” Imefika
    Endeleeni Kukesha!
    • Sasa, kabla “saa ya hukumu” kufikia upeo kwenye uharibifu wa ulimwengu huu mwovu, tunahimizwa hivi: “Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu.” Je, unafanya hivyo? Kufanya hivyo kunahusisha mengi zaidi ya kusema tu “ninamwamini Mungu.” (Mathayo 7:21-23; Yakobo 2:19, 20) Woga unaofaa wa Mungu unapaswa kutufanya tumheshimu. Unapaswa kutufanya tuepuke mabaya. (Methali 8:13) Unapaswa kutusaidia tupende mema na kuchukia mabaya. (Amosi 5:14, 15) Ikiwa tunamheshimu Mungu, tutamsikiliza kwa makini. Hatutaruhusu shughuli nyingine zitufanye tupuuze kusoma Neno lake, Biblia, kwa ukawaida. Tutamtegemea kwa moyo wetu wote nyakati zote. (Zaburi 62:8; Methali 3:5, 6) Wale wanaomheshimu kikweli humtambua kuwa Muumba wa mbingu na dunia, Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote, nao hujitiisha kwake kwa upendo akiwa Mtawala wao. Tukitambua kwamba tunahitaji kuzingatia zaidi mambo haya, tunapaswa kufanya hivyo bila kukawia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki