Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia

      Unahitaji kufanya nini?

      Unahitaji kuwasaidia wasikilizaji wafuatane na wewe unaposoma maandiko ya Biblia.

      Kwa Nini Ni Muhimu?

      Jambo ambalo mtu anaona kwa macho yake, hasa katika Biblia yake mwenyewe, humgusa moyo zaidi.

      KUSUDI letu ni kuelekeza fikira za kila mtu kwenye Neno la Mungu, Biblia. Kitabu hicho kitakatifu ndicho msingi wa ujumbe tunaohubiri, na tunataka watu watambue kwamba yale tunayosema yanatokana na Mungu wala hatusemi mambo yetu wenyewe. Watu wanahitaji kuitumaini Biblia.

      Katika Huduma ya Shambani. Unapojitayarisha kwa ajili ya huduma ya shambani, sikuzote chagua andiko moja au zaidi ambalo utawaonyesha wale walio tayari kusikiliza. Hata kama unapanga kutoa kichapo fulani cha Biblia kwa muda mfupi tu, kwa kawaida ni vizuri kusoma andiko linalofaa la Biblia. Biblia ina uwezo mkubwa wa kuelekeza wenye mfano wa kondoo kuliko jambo jingine lolote ambalo tunaweza kusema. Ikiwa hali hazikuruhusu kusoma Biblia, unaweza kuinukuu. Katika karne ya kwanza, vitabu vya kukunjwa vya Maandiko havikupatikana sana. Hata hivyo, Yesu na mitume wake walinukuu sana Maandiko. Hata sisi tunapaswa kujitahidi kushika Maandiko na kuyatumia vizuri katika huduma yetu, nyakati nyingine tukiyanukuu tu.

      Ikiwa hali zinakuruhusu kusoma Biblia, uishike vizuri ili mwenye nyumba aweze kufuatana nawe unaposoma. Ikiwa mwenye nyumba anafuatana nawe akisoma Biblia yake mwenyewe, yale anayosoma yanaweza kumfanya aitikie kwa njia nzuri zaidi.

      Hata hivyo, ni lazima utambue kwamba baadhi ya watafsiri wa Biblia wamebadili Neno la Mungu. Huenda tafsiri zao hazipatani kwa kila hali na mambo yaliyokuwa katika lugha za awali za Biblia. Tafsiri kadhaa za kisasa zimeondoa jina la Mungu, hazisemi wazi kile ambacho maandishi ya lugha za awali yalisema kuhusu wafu, na zinaficha mafundisho ya Biblia kuhusu kusudi la Mungu kwa dunia. Ili kuonyesha mtu badiliko ambalo limefanywa, mnaweza kuchunguza maandiko hayo katika Biblia tofauti-tofauti au kuchunguza tafsiri za awali za Biblia za lugha iyo hiyo. Kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko kinalinganisha jinsi tafsiri kadhaa zinavyotafsiri maneno makuu ya maandiko ambayo hutumiwa mara nyingi. Mtu yeyote anayependa kweli atafurahi kujua mambo hayo.

  • Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • JINSI YA KUFAULU

      • Onyesha mwenye nyumba andiko unalosoma katika Biblia, au umwombe atumie Biblia yake kufuatana nawe unaposoma.

  • Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • MAZOEZI: Katika ziara za kurudia, jaribu kutumia njia zinazofuata: (1) Mpe mwenye nyumba Biblia yako, mwulize kama angependa kusoma andiko ambalo umechagua. (2) Mwulize kama angependa kuleta Biblia yake mwenyewe na kusoma andiko fulani kuu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki