-
Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini ZoteHuduma ya Ufalme—1998 | Februari
-
-
19 Katika sehemu fulani za mji mkuu za Afrika Mashariki, kumekuwa na Wachina kadhaa ambao huamini Ubuddha na falsafa nyinginezo za Kimashariki. Wengi wanafanya kazi katika miradi tofauti-tofauti. Kwa mfano, dada mmoja katika Montana, Marekani, alipomwona mwanamume Mchina katika duka la kuuzia mboga, alimpa trakti katika lugha yake na kumtolea funzo la Biblia. Yeye alisema: “Wamaanisha Biblia Takatifu? Nimekuwa nikiitafuta maishani mwangu mwote!” Alianza kujifunza juma hilo na kuanza kuhudhuria mikutano yote. Vivyo hivyo, wahubiri fulani katika eneo letu wameweza kuanzisha mafunzo ya Biblia na Wachina fulani.
20 Kwa muda wa zaidi ya mwongo moja, dada painia katika Nevada amekuwa akifundisha wanafunzi Wachina kweli. Alipokuwa akihubiri jengo moja lililokuwa na vyumba vinane vilivyokaliwa na wanafunzi hawa, alisali kwa Yehova amsaidie kuanzisha funzo katika kila chumba. Katika majuma mawili alikuwa akijifunza na angalau mwanafunzi mmoja katika kila chumba. Mfikio ufanyao kazi vizuri kwake ni kusema kwamba amepata miongoni mwa wanafunzi hao hangaiko moja linalofanana—wote wanataka amani na furaha. Kisha yeye huuliza kama hilo ni hangaiko lao pia. Sikuzote wao hukubali. Yeye huelekeza uangalifu wao kwenye broshua Lasting Peace and Happiness—How to Find Them, ambayo imekusudiwa Wachina. Baada ya kujifunza masomo matano tu, mwanafunzi mmoja alimwambia amekuwa akitafuta kweli kwa muda mrefu na sasa ameipata.
-
-
Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini ZoteHuduma ya Ufalme—1998 | Februari
-
-
Wachina
Lasting Peace and Happiness—How to Find Them (Broshua)
-