Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini Zote
    Huduma ya Ufalme—1998 | Februari
    • 25 Kutoa Ushahidi kwa Waislamu: (Ona Sura ya 12 katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.) Waislamu, ni wafuasi wa Uislamu (au, Umuhammad), ambao hutia ndani itikadi katika Allah kuwa mungu wao wa pekee na katika Muhammad (570-632 W.K.) kuwa nabii wake wa mwisho na wa maana zaidi. Kwa sababu hawaamini kwamba Mungu alikuwa na mwana, Waislamu humtambua Yesu Kristo kuwa nabii mdogo zaidi wa Mungu, lakini si zaidi ya hilo. Kurani, ambacho ni kitabu chenye miaka isiyozidi 1,400, hutaja Maandiko ya Kiebrania na pia ya Kigiriki. Ufanani mkubwa upo kati ya Uislamu na Ukatoliki. Dini zote mbili hufundisha hali ya kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu, hali ya mateso ya muda tu, na kuwako kwa helo yenye kuwaka moto.

      26 Masikilizano yaliyo wazi katika itikadi yetu ni kwamba kuna Mungu mmoja tu wa kweli na kwamba Biblia ilipuliziwa naye. Msomaji mwangalifu wa Kurani ameona marejezeo kwenye Torah, Zaburi, na Gospeli kuwa Neno la Mungu na amesoma kwamba vitabu hivyo vyapasa kutambuliwa kuwa hivyo na kutiiwa. Kwa sababu hiyo, waweza kujitoa kujifunza vitabu hivyo na mtu huyo.

      27 Utoaji huu waweza kufanya kazi kwa mtu anayejitambulisha kuwa Mwislamu: “Sijaongea na Waislamu wengi, lakini nimesoma jambo fulani juu ya mafundisho machache ya dini yenu katika kitabu hiki chenye kubebeka kwa urahisi. [Fungua ukurasa wa 24 katika kitabu Kutoa Sababu.] Kinasema nyinyi huamini kwamba Yesu alikuwa nabii lakini kwamba Muhammad alikuwa nabii wa mwisho na wa maana zaidi. Je, waamini pia kwamba Musa alikuwa nabii wa kweli? [Ruhusu itikio.] Je, naweza kukuonyesha jambo ambalo Musa alijifunza kutoka kwa Mungu kuhusu jina Lake la kibinafsi?” Kisha usome Kutoka 6:2, 3. Katika ziara ya kurudia, unaweza kuzungumzia kichwa kidogo “Mungu Mmoja, Dini Moja,” kwenye ukurasa wa 13 katika kijitabu Sasa Ndio Wakati wa Kumtii Mungu Kweli Kweli.

  • Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini Zote
    Huduma ya Ufalme—1998 | Februari
    • Waislamu

      Jinsi ya Kuipata Barabara ya Kwenda Kwenye Paradiso (Trakti)

      Sasa Ndio Wakati wa Kumtii Mungu Kweli Kweli (Kijitabu)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki