Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tumia kwa Ustadi “Upanga wa Roho”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Februari 15
    • Litumie Neno la Mungu kwa Ushawishi

      14. Kuwashawishi wasikilizaji kunamaanisha nini?

      14 Kutumia Biblia kwa ustadi katika huduma hakumaanishi kunukuu tu maandiko. Paulo alizungumza kwa “ushawishi,” na tunapaswa pia kufanya hivyo. (Soma Matendo 19:8, 9; 28:23.) Neno “shawishi” linamaanisha “sadikisha.” Yule anayeshawishiwa “anasadikishwa kabisa mpaka aamini jambo fulani.” Tunapomshawishi mtu akubali fundisho la Biblia, tunamsadikisha ili aamini fundisho hilo. Ili kufanya hivyo, tunahitaji kumsadikisha msikilizaji kwamba tunasema kweli. Tunaweza kufanya hivyo kwa njia zifuatazo.

      15. Unaweza kuelekeza uangalifu kwenye Biblia jinsi gani ili iheshimiwe?

      15 Elekeza uangalifu kwenye Neno la Mungu kwa njia inayofanya liheshimiwe. Kabla ya kusoma andiko, kazia kwa nini ni jambo la maana kujua maoni ya Mungu kuhusu jambo mnalozungumzia. Baada ya kuuliza swali na mwenye-nyumba kujibu, unaweza kusema hivi: ‘Acha tuone maoni ya Mungu kuhusu jambo hili.’ Au unaweza kuuliza, ‘Mungu anasema nini kuhusu jambo hili?’ Unaposema hivyo kabla ya kusoma andiko unakazia kwamba Biblia iliongozwa na Mungu na hivyo unamfanya msikilizaji aiheshimu sana. Ni jambo la maana kufanya hivyo hasa tunapomhubiria mtu ambaye anamwamini Mungu lakini hajui Biblia inafundisha nini.—Zab. 19:7-10.

      16. Ni nini kitakachokusaidia kueleza maana ya maandiko kwa njia inayofaa?

      16 Usisome tu maandiko; eleza maana yake. Paulo alikuwa na desturi ya ‘kueleza na kuthibitisha kwa marejeo’ mambo aliyofundisha. (Mdo. 17:3) Kwa kawaida, andiko la Biblia lina masomo mbalimbali, na hivyo, huenda ukahitaji kukazia maneno makuu ambayo yanahusiana na jambo mnalozungumzia. Unaweza kufanya hivyo kwa kurudia maneno yanayokazia wazo kuu au unaweza kuuliza maswali ambayo yatamsaidia mwenye-nyumba kuyatambua. Kisha, eleza maana ya sehemu hiyo ya andiko. Baada ya kufanya hivyo, msaidie msikilizaji aone jinsi andiko hilo linavyomhusu yeye binafsi.

      17. Unaweza kutumia Maandiko jinsi gani kujadiliana kwa njia yenye kusadikisha?

      17 Tumia Maandiko kujadiliana kwa njia yenye kusadikisha. Paulo ‘alijadiliana na wengine kwa kutumia Maandiko’ huku akitumia hoja zenye kusadikisha na kuwasihi kutoka moyoni. (Mdo. 17:2, 4) Jitahidi kugusa moyo wa mtu anayekusikiliza kama Paulo alivyofanya. ‘Teka’ mambo yaliyo moyoni mwake kwa kutumia maswali yenye fadhili ambayo yanaonyesha kwamba unamjali kikweli mtu huyo. (Met. 20:5) Usizungumze bila kujali. Toa hoja zako kwa njia iliyo wazi na yenye kueleweka. Unapaswa kutegemeza hoja hizo kwa uthibitisho wenye kuridhisha. Mambo unayosema yanapaswa kutegemea kabisa Neno la Mungu. Ni afadhali kufafanua vizuri andiko moja na kutumia mfano kuonyesha matumizi yake, badala ya kusoma maandiko mawili au matatu haraka-haraka. Kutumia uthibitisho wa ziada kunaweza pia ‘kuongeza ushawishi kwenye midomo yetu.’ (Met. 16:23) Nyakati nyingine, huenda ikafaa kufanya utafiti na kupata habari za ziada. Yule mwanamke mwenye umri wa miaka 93 aliyetajwa mwanzoni alitaka kujua kwa nini fundisho la kutokufa kwa nafsi (au roho) limeenea sana. Ili ashawishiwe kukubali fundisho la Biblia kuhusu jambo hilo, alihitaji kuelewa chanzo cha fundisho hilo na jinsi lilivyoingizwa katika dini nyingi ulimwenguni.b

  • Tumia kwa Ustadi “Upanga wa Roho”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Februari 15
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 12]

      Jinsi ya Kutumia Neno la Mungu kwa Ushawishi

      ▪ Itumie Biblia kwa njia inayofanya iheshimiwe

      ▪ Eleza maana ya Maandiko

      ▪ Jadiliana na watu kwa njia yenye kusadikisha ili uguse mioyo yao

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki