Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ana Maoni Gani Kuhusu Visingizio?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • Visingizio Ambavyo Havikubaliwi na Mungu

      “Ni vigumu sana.” Hasa kwa wale ambao kiasili ni waoga, huenda likaonekana kuwa jambo gumu sana kwao kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Hata hivyo, ona yale tunayoweza kujifunza kutokana na mfano wa Yona. Alipewa mgawo ambao aliuona kuwa mgumu sana—Yehova alimwambia atangaze uharibifu wa Ninawi uliokuwa ukija. Si vigumu kuelewa kwa nini Yona aliogopa sana kutimiza mgawo huo. Ninawi ulikuwa mji mkuu wa nchi ya Ashuru, na Waashuru walijulikana kuwa wakatili sana. Huenda Yona alijiuliza: ‘Nitafaulu jinsi gani katikati ya watu hao? Watanitendea namna gani?’ Muda mfupi baadaye, alikimbia. Hata hivyo, Yehova hakukubali kisingizio cha Yona. Badala yake, Yehova alimtuma tena kwenda kuwahubiria Waninawi. Wakati huu, Yona alitimiza mgawo wake kwa uhodari, na Yehova alibariki matokeo ya kazi yake.—Yona 1:1-3; 3:3, 4, 10.

      Ikiwa unafikiri kwamba mgawo wa kuhubiri habari njema ni mgumu sana kwako, kumbuka kwamba “mambo yote yanawezekana kwa Mungu.” (Marko 10:27) Unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atakutia nguvu ukiendelea kumwomba akusaidie na kwamba atakubariki unapojitahidi kupata uhodari ili kutimiza huduma yako.—Luka 11:9-13.

  • Yehova Ana Maoni Gani Kuhusu Visingizio?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • “Sina uwezo.” Huenda ukahisi kwamba hustahili kuwa mhudumu wa habari njema. Watumishi fulani waaminifu wa Yehova katika nyakati za Biblia walihisi kwamba hawakuwa na uwezo wa kutimiza migawo ambayo Yehova aliwapa. Fikiria mfano wa Musa. Alipopewa kazi ya pekee na Yehova, Musa alisema hivi: “Nakuomba radhi, Yehova, lakini mimi si msemaji mzuri, tangu jana wala tangu kabla ya hapo wala tangu uliposema na mtumishi wako, kwa maana kinywa changu ni kizito na ulimi wangu ni mzito.” Ingawa Yehova alimpa uhakikisho, Musa alijibu: “Nakuomba radhi, Yehova, lakini tuma, tafadhali, kupitia mkono wa yule utakayemtuma.” (Kut. 4:10-13) Yehova alitenda jinsi gani?

      Yehova hakukubali visingizio vya Musa vya kukataa kutimiza mgawo huo. Hata hivyo, Yehova alimweka rasmi Haruni ili amsaidie Musa kutimiza mgawo huo. (Kut. 4:14-17) Zaidi ya hayo, katika miaka iliyofuata, Yehova alimtegemeza Musa na kumpa chochote alichohitaji ili kufanikiwa katika kutimiza migawo aliyopewa na Mungu. Leo, unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atawachochea waamini wenzako wenye uzoefu wakusaidie pia ili utimize huduma yako. Zaidi ya yote, Neno la Mungu linatuhakikishia kwamba Yehova atatuwezesha tuwe na sifa zinazostahili ili tutimize kazi ambayo ametuamuru kufanya.—2 Kor. 3:5; ona sanduku “Miaka Yenye Furaha Zaidi Katika Maisha Yangu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki