-
Iga Mfano Ambao Yesu Aliweka Katika KukeshaMnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
-
-
5, 6. (a) Ujuzi wetu kuhusu wakati ujao na makusudi ya Mungu unatusaidiaje kuendelea kukesha? (b) Kwa nini mambo tunayojua kumhusu Shetani yanapaswa kutufanya tuazimie zaidi kuendelea kukesha?
5 Kwa upande mwingine, Yesu alijua mambo mengi mazuri ajabu kuhusu wakati ujao, kweli ambazo watu wengi wa siku zake hawakuzijua kamwe. Hatujui mambo mengi hivyo kama Yesu, lakini kupitia mafundisho yake, tunajua mambo mengi kuhusu Ufalme wa Mungu na yale ambayo utatimiza hivi karibuni. Tunapowatazama watu wanaotuzunguka, shuleni, kazini, au katika eneo tunalohubiri, je, hatuoni kwamba wengi wao wanaishi katika giza zito la kiroho kwa sababu ya kutojua kweli hizo nzuri ajabu? Hiyo ni sababu nyingine inayotufanya tuendelee kukesha. Kama Yesu, tunahitaji kuwa macho sikuzote, kwa kutumia fursa zote tunazopata ili kuwaambia wengine mambo tunayojua kuhusu Ufalme wa Mungu. Kila fursa tunayopata ni yenye thamani, na hatutaki kupoteza fursa yoyote ile. Uhai wa watu uko hatarini!—1 Tim. 4:16.
-
-
Iga Mfano Ambao Yesu Aliweka Katika KukeshaMnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
-
-
JINSI YA KUENDELEA KUKESHA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI
10. Ni mfano gani unaotuonyesha kwamba Yesu alikuwa macho kutumia fursa alizopata ili kutoa ushahidi?
10 Yesu aliendelea kukesha katika kazi aliyopewa na Yehova afanye. Huenda kukawa na kazi fulani ambazo zinaweza kuruhusu akili ya mfanyakazi kutanga-tanga bila madhara yoyote. Hata hivyo, kazi nyingi zinahitaji mtu kuwa makini na kubaki macho, na bila shaka huduma ya Kikristo inahitaji hivyo. Yesu alikuwa macho sikuzote katika kazi yake, akitafuta fursa mbalimbali ili kuhubiri habari njema. Kwa mfano, wakati yeye na wanafunzi wake walipofika katika mji wa Sikari baada ya kutembea asubuhi yote, wanafunzi walienda kununua chakula. Yesu alibaki kando ya kisima cha mji ili kupumzika, lakini alikuwa macho na aliona fursa ya kutoa ushahidi. Mwanamke Msamaria alikuja kuchota maji. Yesu angeamua kulala kidogo au angefikiria sababu nyingine za kutozungumza na mwanamke huyo. Hata hivyo, alianzisha mazungumzo na mwanamke huyo, na akamtolea ushahidi wenye nguvu ambao ulisaidia watu wengi katika jiji hilo. (Yoh. 4:4-26, 39-42) Je, tunaweza kuiga kwa ukaribu zaidi mfano wa Yesu katika kukesha, labda kwa kujitahidi kuwa macho zaidi ili kutumia fursa tunazopata kuwahubiria habari njema watu tunaokutana nao kila siku?
-