-
Njia za Kuhubiri Habari NjemaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
ukiwatembelea tena. Unapozungumza nao habari zaidi kuhusu Biblia, unaweza kuimarisha imani yao katika Mungu na kuwasaidia kutambua uhitaji wao wa kiroho. (Mt. 5:3) Ukipanga kurudi wakati unaofaa na ukijitayarisha vizuri, huenda ukaanzisha funzo la Biblia. Unapaswa kuwa na lengo hilo unapofanya ziara za kurudia. Sisi hupanda mbegu ya kweli na vilevile kuitia maji.—1 Kor. 3:6.
15 Huenda ikawa vigumu kwa wengine kufanya ziara za kurudia. Labda umezoea kuhubiri kifupi habari njema na unafurahia kufanya hivyo. Lakini huenda ukaogopa kumrudia mwenye nyumba ili kuendeleza mazungumzo ya Biblia. Matayarisho mazuri yatakusaidia kuwa na ujasiri. Tumia mapendekezo yanayotolewa katika mkutano wa katikati ya juma. Pia, unaweza kupanga kuhubiri na mhubiri mwenye uzoefu ili akusaidie.
KUONGOZA MAFUNZO YA BIBLIA
16 Alipokuwa akizungumza na mtu aliyegeuzwa imani na kuwa Myahudi ambaye alikuwa akisoma Neno la Mungu, mweneza-injili Filipo alimwuliza hivi: “Je, kweli unajua unayosoma?” Mwanamume huyo alijibu: “Kwa kweli, ninawezaje kuyaelewa mtu fulani asiponiongoza?” Masimulizi ya Biblia kwenye Matendo sura ya 8 yanaeleza kwamba Filipo ‘alimtangazia habari njema kumhusu Yesu,’ akianza na andiko ambalo mtu huyo alikuwa akisoma. (Mdo. 8:26-36) Hatujui Filipo alizungumza naye kwa muda gani, lakini Filipo alimweleza waziwazi habari njema hivi kwamba mtu huyo akaamini na akaomba kubatizwa. Kisha akawa mwanafunzi wa Yesu Kristo.
17 Watu wengi leo hawajui mafundisho ya Biblia, na huenda tukahitaji kuwarudia mara nyingi na kujifunza nao kwa majuma au miezi kadhaa, au hata mwaka mmoja au zaidi ili wawe na imani na wastahili kubatizwa. Hata hivyo, ukiwasaidia kwa subira na upendo watu wanyofu wawe wanafunzi, utapata thawabu kama Yesu alivyosema: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Mdo. 20:35.
18 Bila shaka, ungependa kuongoza funzo la Biblia ukitumia machapisho yaliyotayarishwa kwa kusudi hilo. Kwa kutumia maagizo yanayotolewa kwenye mkutano wa katikati ya juma na kwa kuhubiri na walimu wenye uzoefu kutanikoni, utafaulu kuongoza mafunzo yenye matokeo, na kuwasaidia wengine wawe wanafunzi wa Yesu Kristo.
19 Ikiwa unahitaji kusaidiwa kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia, zungumza na mzee yeyote au Shahidi mwenye ustadi wa kuongoza mafunzo ya Biblia. Mapendekezo yanayopatikana katika Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha na ambayo huzungumziwa kwenye mkutano huo yatakusaidia pia. Mtegemee Yehova na usali kuhusu tamaa yako ya kuongoza funzo. (1 Yoh. 3:22) Kwa hiyo, jitahidi kuongoza angalau funzo moja la Biblia mbali na funzo ambalo huenda unaongoza katika familia yako. Ukiongoza mafunzo ya Biblia, utapata shangwe zaidi katika huduma.
KUWAELEKEZA WANAOPENDEZWA KWENYE TENGENEZO LA YEHOVA
20 Tunapowasaidia watu wamjue Yehova Mungu na kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, wanajiunga na kutaniko. Wanafunzi wa Biblia watafanya maendeleo ya kiroho na kukomaa ikiwa watalifahamu tengenezo la Yehova na kushirikiana nalo. Ni muhimu tuwafundishe jinsi ya kufanya hivyo. Unaweza kuwasaidia kwa kutumia broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? na video zilizotayarishwa kwa kusudi hilo. Unaweza pia kutumia habari iliyo katika Sura ya 4 ya kitabu hiki.
21 Mara tu mnapoanza kujifunza Biblia, msaidie mwanafunzi aone kwamba Yehova anatumia tengenezo kutimiza kazi ya kuhubiri inayoendelea duniani. Mweleze faida za machapisho ya kujifunzia Biblia na jinsi yanavyotayarishwa na kusambazwa ulimwenguni pote na wafanyakazi wa kujitolea ambao wamejiweka wakfu kwa Mungu. Mwalike mwanafunzi wako wa Biblia mwende pamoja kwenye Jumba la Ufalme. Mweleze jinsi mikutano inavyofanywa na umtambulishe kwa akina ndugu na dada. Msaidie pia afahamiane na Mashahidi wengine kwenye makusanyiko. Katika pindi hizo, mwache mwanafunzi ajionee jinsi waabudu wa Yehova wanavyopendana, jambo linalowatambulisha Wakristo wa kweli. (Yoh. 13:35) Mtu anayependezwa akiendelea kulithamini tengenezo la Yehova, atazidi kumkaribia Yehova.
KUTUMIA MACHAPISHO YA BIBLIA
22 Wakristo wa karne ya kwanza walihubiri kwa bidii Neno la Mungu. Walinakili kwa mkono Maandiko waliyotumia kujifunza wao binafsi na kutanikoni. Waliwahimiza watu wasome Neno la Mungu la kweli. Nakala walizonakili zilikuwa chache na hivyo walizithamini sana. (Kol. 4:16; 2 Tim. 2:15; 3:14-17; 4:13; 1 Pet. 1:1) Leo, Mashahidi wa Yehova hutumia mbinu za kisasa kuchapisha mamia ya mamilioni ya Biblia na machapisho ya kujifunzia Biblia. Machapisho hayo yanatia ndani trakti, broshua, vitabu, na magazeti katika lugha nyingi.
23 Unapowahubiria wengine habari njema, tumia machapisho ya kujifunzia Biblia yanayoandaliwa na tengenezo la Yehova. Unapotafakari jinsi ambavyo umefaidika kwa kusoma na kujifunza machapisho ya Mashahidi wa Yehova, utachochewa kuwapa wengine pia.—Ebr. 13:15, 16.
24 Watu wengi sana hutegemea kupata habari katika Intaneti. Kwa hiyo, mbali na machapisho ya Biblia, tovuti yetu rasmi ya jw.org ni njia nyingine nzuri ya kutangaza habari njema. Watu ulimwenguni pote wanaweza kutumia kompyuta zao kusoma au kusikiliza Biblia na machapisho ya Biblia yakisomwa katika mamia ya lugha. Watu wanaosita kuzungumza nasi au wanaoishi katika maeneo ambayo hayana Mashahidi wengi wa Yehova wanaweza kuchunguza mambo tunayoamini kwa kutumia jw.org wakiwa nyumbani kwao.
25 Kwa hiyo, tunawajulisha watu kuhusu jw.org kila tunapopata fursa. Mwenye nyumba anapouliza swali kuhusu imani yetu, tunaweza kutumia simu au kompyuta kumwonyesha jibu papo hapo. Tunapokutana na mtu anayezungumza lugha nyingine, kutia ndani lugha ya alama, tunaweza kumwelekeza kwenye tovuti yetu ili asome Biblia na machapisho ya Biblia katika lugha yake. Wahubiri wengi wametumia mojawapo ya video zilizo kwenye tovuti hiyo kuanzisha mazungumzo ya Biblia.
MAHUBIRI YASIYO RASMI
26 Yesu aliwaambia hivi wale waliokuwa wakimsikiliza: “Ninyi ndio nuru ya ulimwengu. . . . Acheni nuru yenu iangaze mbele ya watu, ili waone matendo yenu mema na kumtukuza Baba yenu aliye mbinguni.” (Mt. 5:14-16) Wanafunzi hao waliishi kulingana na viwango vya Mungu kwa kumwiga Yesu aliyesema: “Mimi ndiye nuru ya ulimwengu.” Yesu aliwawekea Wakristo mfano kwa kuacha “nuru ya uzima” iangaze kwa faida ya wote ambao wangesikiliza.—Yoh. 8:12.
27 Mtume Paulo pia alituwekea mfano mzuri. (1 Kor. 4:16; 11:1) Alipokuwa Athene, kila siku aliwahubiria watu aliokutana nao sokoni. (Mdo. 17:17) Wakristo huko Filipi waliiga mfano wake. Kwa sababu hiyo, Paulo aliwaandikia hivi: Mnaishi “katikati ya kizazi kilicho kombo na kilichopotoka, ambao kati yao mnaangaza kama mianga katika ulimwengu.” (Flp. 2:15) Sisi pia tunaweza kuacha kweli ya Ufalme iangaze kupitia maneno na matendo yetu tunapopata nafasi ya kuwaambia wengine habari njema. Ni kweli kwamba mfano wetu mzuri wa kuwa wanyofu na waadilifu unaweza kuonyesha sisi ni tofauti na ulimwengu. Hata hivyo, tukizungumza na watu kuhusu habari njema, watajua sababu inayotufanya tuwe tofauti.
28 Mashahidi wengi wa Yehova huwahubiria habari njema watu wanaokutana nao kila siku kazini, shuleni, kwenye usafiri wa umma, au katika shughuli zao za kila siku. Tunaposafiri, tunaweza kuzungumza na wasafiri wenzetu. Kila mmoja wetu anapaswa kuwa tayari kutoa ushahidi katika mazungumzo yoyote ya kawaida. Acheni tuwe tayari kuzungumza na wengine wakati wowote.
29 Tutachochewa kuzungumza na wengine tukikumbuka kwamba kwa kufanya hivyo tunamsifu Muumba wetu na kuliheshimu jina lake. Isitoshe, tunaweza kuwasaidia watu wenye moyo mnyoofu wamjue Yehova ili wao pia wamtumikie na kuwa na tumaini la kupata uzima kwa msingi wa imani katika Yesu Kristo. Yehova hupendezwa sana na jitihada hizo na kuuona huo kuwa utumishi mtakatifu.—Ebr. 12:28; Ufu. 7:9,10.
ENEO
30 Mapenzi ya Yehova ni kwamba ujumbe wa Ufalme uhubiriwe kwa utaratibu ulimwenguni pote, mijini na vijijini. Ili kutimiza hilo, makutaniko na watu binafsi wanaohubiri maeneo ya mbali hupewa eneo na ofisi ya tawi. (1 Kor. 14:40) Hilo linapatana na mpango wa Mungu uliofuatwa katika karne ya kwanza. (2 Kor. 10:13; Gal. 2:9) Kazi ya kuhubiri Ufalme inapopanuka haraka katika siku hizi za mwisho, tutapata matokeo mazuri ikiwa kuna utaratibu mzuri wa kuhubiri maeneo ya kutaniko.
31 Mwangalizi wa utumishi ndiye anayesimamia mipango hiyo. Mtumishi wa huduma anaweza kuwagawia wahubiri maeneo. Kuna aina mbili za maeneo, maeneo ya vikundi na maeneo ya kibinafsi ya wahubiri. Katika kutaniko lenye eneo dogo, waangalizi wa vikundi huwa na maeneo ambayo huhubiriwa na wahubiri wa vikundi vyao. Katika kutaniko lenye eneo kubwa, wahubiri wanaweza kupewa eneo la kibinafsi.
32 Mhubiri aliye na eneo la kibinafsi anaweza kuhubiri eneo hilo wakati ambapo hakuna mpango wa mkutano wa utumishi wa shambani au kama hawezi kufika kwenye kikundi. Kwa mfano, wahubiri fulani huchukua eneo lililo karibu na mahali wanapofanya kazi nao huhubiri wakati wa mapumziko ya mchana au baada ya kazi. Familia fulani huchukua eneo la kibinafsi karibu na nyumbani kwao na kuhubiri wakati wa jioni. Kuwa na eneo la kibinafsi lililo karibu humsaidia mhubiri atumie wakati mwingi zaidi katika utumishi wa shambani. Eneo la kibinafsi linaweza pia kuhubiriwa na kikundi. Kama ungependa kuwa na eneo la kibinafsi unaweza kumwomba mtumishi wa maeneo.
33 Iwe ni eneo la kikundi lililopewa mwangalizi wa kikundi au eneo la kibinafsi lililopewa mhubiri, mtu aliyepewa eneo hilo atajitahidi kadiri awezavyo kuzungumza na mtu fulani katika kila nyumba. Mipango ya kuhubiri eneo kikamili inapaswa kufuata sheria za kulinda taarifa zinazotumiwa. Kila mwangalizi wa kikundi au mhubiri anayepewa eneo anapaswa kujitahidi kulikamilisha kwa miezi minne. Mara tu anapomaliza, anapaswa kumjulisha mtumishi wa maeneo. Ikitegemea na hali, mwangalizi wa kikundi au mhubiri anaweza kubaki na eneo hilo ili alihubiri tena au anaweza kumrudishia mtumishi wa maeneo.
34 Wahubiri wote kutanikoni wakishirikiana, eneo linaweza kuhubiriwa kikamili. Pia, eneo moja halitahubiriwa na wahubiri tofauti-tofauti wakati uleule, jambo linaloweza kuwaudhi wenye nyumba. Tukifanya hivyo, tutaonyesha kwamba tunawajali ndugu zetu na watu walio katika eneo.
KUSHIRIKIANA KUWAHUBIRIA WATU WA KILA LUGHA
35 Wanadamu wote wanahitaji kujifunza kumhusu Yehova Mungu, Mwana wake, na Ufalme. (Ufu. 14:6, 7) Tungependa kuwasaidia watu wa lugha zote waliitie jina la Yehova ili waokolewe na wavae utu mpya wa Kikristo. (Rom. 10:12, 13; Kol. 3:10, 11) Tunakabili changamoto gani tunapohubiri maeneo yenye watu wanaozungumza lugha mbalimbali? Tunawezaje kukabiliana na hali hizo ili watu wengi iwezekanavyo wasikie ujumbe wa Ufalme katika lugha wanayoelewa vizuri?—Rom. 10:14.
36 Maeneo hupangwa kulingana na lugha. Kwa hiyo, wahubiri wa makutaniko yenye maeneo ya lugha tofauti-tofauti wanaweza kuhubiri eneo lilelile. Katika maeneo hayo, ni vizuri wahubiri wa kila kutaniko wajitahidi kuwahubiria watu wanaozungumza lugha ya kutaniko lao. Hilo linahusika pia wakati wa kampeni za kila mwaka za kugawa mialiko. Hata hivyo, wahubiri wanapohubiri hadharani na isivyo rasmi, wanaweza kuzungumza na mtu yeyote na kutoa machapisho ya lugha yoyote.
37 Katika visa fulani, makutaniko ya lugha tofauti yanaweza kushindwa kuhubiri kikamili maeneo yao kwa ukawaida. Katika visa kama hivyo, waangalizi wa utumishi wa makutaniko yanayohusika wanapaswa kuwasiliana ili kupanga utaratibu unaofaa wa kuhubiri eneo lote. Hilo litampa kila mtu nafasi ya kusikia ujumbe wa Ufalme na kuzuia makutaniko tofauti kuhubiri eneo lilelile kwa wakati mmoja.—Met. 15:22.
38 Tunapaswa kufanya nini ikiwa mwenye nyumba anazungumza lugha tofauti? Tusifikiri kwamba wahubiri wanaozungumza lugha yake watamtembelea. Wahubiri fulani wamejifunza utangulizi mfupi wa lugha zinazozungumzwa katika eneo lao. Tunaweza kumwonyesha mtu jinsi ya kusoma au kupakua machapisho ya lugha yake kwenye tovuti yetu rasmi ya jw.org, au tunaweza kupanga kumletea machapisho ya lugha yake.
39 Mwenye nyumba akionyesha upendezi, tunapaswa kujaribu kumtafuta mhubiri anayezungumza lugha anayoelewa. Pia tunaweza kumwelekeza kwenye kutaniko la karibu linalofanya mikutano kwa lugha yake. Ikiwa anapenda kuwasiliana na mhubiri anayezungumza lugha yake, tunaweza kumwelekeza jinsi ya kujaza habari zake za mawasiliano kwenye Tovuti ya jw.org. Kisha, ofisi ya tawi itajitahidi kupata mhubiri aliye karibu, kikundi, au kutaniko linaloweza kumsaidia zaidi.
40 Tunapaswa kuendelea kumtembelea mtu huyo anayependezwa mpaka atakapotembelewa na mhubiri anayezungumza lugha yake. Katika visa fulani, huenda ofisi ya tawi ikawajulisha wazee kwamba hawakumpata mhubiri anayezungumza lugha ya mtu huyo. Ikiwa ndivyo, tunapaswa kujitahidi kuendeleza upendezi wa mwenye nyumba. Ikiwezekana tunaweza kujifunza naye Biblia, labda kwa kutumia machapisho ya lugha yake. Tukitumia vizuri picha na kumwomba mtu huyo asome maandiko yaliyonukuliwa, atapata ujuzi fulani wa msingi wa Biblia. Labda ana mtu wa ukoo anayejua lugha yake na lugha ya kutaniko ambaye anaweza kumtafsiria ujumbe.
41 Ili kumwelekeza mtu anayependezwa kwenye tengenezo la Mungu, tunapaswa kumwalika ahudhurie mikutano yetu, ingawa huenda asielewe kikamili mambo yanayozungumziwa. Maandiko yanaposomwa, tunaweza kumsaidia kuyapata katika Biblia ya lugha yake ikiwa inapatikana. Anaposhirikiana na wengine kutanikoni, anaweza kuimarishwa na kusaidiwa kufanya maendeleo zaidi ya kiroho.
42 Vikundi vidogo: Kikundi kidogo hufanyizwa na wahubiri wanaotumia lugha tofauti na ile inayotumiwa na kutaniko lao, ingawa hakuna mzee au mtumishi wa huduma anayestahili kuongoza mikutano katika lugha hiyo kila juma. Ofisi ya tawi inaweza kutambua kutaniko kuwa linalosimamia kikundi kidogo ikiwa matakwa yafuatayo yametimizwa:
(1) Kuna idadi ya kutosha ya watu katika eneo ambao wanazungumza lugha nyingine tofauti na lugha ya kutaniko.
(2) Angalau kuna wahubiri wachache wanaojua au wako tayari kujifunza lugha hiyo.
(3) Baraza la wazee liko tayari kuongoza mipango ya mahubiri katika lugha hiyo.
Ikiwa baraza la wazee liko tayari kusimamia kikundi kidogo, wazee wanapaswa kuwasiliana na mwangalizi wa mzunguko. Huenda anajua makutaniko mengine yanayojitahidi kuwahubiria watu wa lugha hiyo na anaweza kuandaa habari muhimu itakayowasaidia kujua kutaniko linaloweza kusimamia kikundi hicho kidogo kwa njia bora zaidi. Baada ya kuamua ni kutaniko gani litakalosimamia, wazee wanaweza kuandika barua kwa ofisi ya tawi na kuomba idhini ya kutambuliwa rasmi kama kutaniko linalosimamia kikundi kidogo.
43 Vikundi: Ofisi ya tawi inaweza kutambua kutaniko kuwa linalosimamia kikundi ikiwa matakwa yafuatayo yametimizwa:
(1) Kuwe na idadi ya kutosha ya watu wanaopendezwa na uwezekano wa ongezeko katika eneo la lugha hiyo.
(2) Angalau idadi ndogo ya wahubiri wanaozungumza au wanaojifunza lugha hiyo.
(3) Mzee au mtumishi wa huduma anayestahili anapatikana ili kusimamia na kuongoza angalau mkutano mmoja katika juma—au sehemu ya mkutano wa kila juma, kama vile hotuba ya watu wote au Funzo la Mnara wa Mlinzi—katika lugha hiyo.
Matakwa hayo yanapotimizwa kwa kiwango kinachofaa, baraza la wazee litaandikia ofisi ya tawi barua yenye habari kamili na kuomba kutambuliwa rasmi kuwa kutaniko linalosimamia kikundi. Mzee au mtumishi wa huduma anayesimamia kikundi hicho ataitwa “mwangalizi wa kikundi” au “mtumishi wa kikundi” akiwa na jukumu la kutunza kikundi hicho.
44 Baada ya kikundi kuanzishwa, baraza la wazee la kutaniko linalosimamia kikundi hicho litaamua ikiwa sehemu nyingine za mikutano ya kutaniko zinapaswa kuongezwa na ni mara ngapi kwa mwezi zinapaswa kufanywa. Mikutano ya utumishi wa shambani inaweza pia kupangwa kwa ajili ya kikundi hicho. Washiriki wote watakuwa chini ya usimamizi wa baraza la wazee linalotegemeza kikundi hicho. Wazee watatoa mwongozo wenye usawaziko na kuchukua hatua zifaazo ili kushughulikia mahitaji ya kikundi hicho. Mwangalizi wa mzunguko anapohubiri pamoja na kikundi hicho katika juma la ziara yake kwa kutaniko linalotegemeza, ataandikia ofisi ya tawi ripoti fupi kuhusu maendeleo ya kikundi hicho na kutaja mahitaji hususa. Baada ya muda, huenda kikundi hicho kikastahili kuwa kutaniko. Ikiwa wote wanaohusika wanafuata miongozo ya kitheokrasi, Yehova atafurahi.—1 Kor. 1:10; 3:5, 6.
MAHUBIRI YA VIKUNDI
45 Kila Mkristo aliyejiweka wakfu ana wajibu wa kuwahubiria wengine habari njema. Kuna njia nyingi za kufanya hivyo, lakini wengi wetu hufurahia kuhubiri pamoja na wahubiri wengine. (Luka 10:1) Kwa hiyo, makutaniko hukutana kwa ajili ya utumishi wa shambani katika mwisho juma na pia katikati ya juma. Kunapokuwa na sikukuu, tunapata pia nafasi za kuhubiri tukiwa kikundi, kwa kuwa ndugu wengi hawaendi kazini. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko hupanga mahali pa mikutano ya utumishi wa shambani na wakati unaowafaa wengi wakati wa mchana na jioni.
46 Mahubiri ya vikundi huwasaidia wahubiri kufanya kazi pamoja na hivyo ‘kutiana moyo.’ (Rom. 1:12) Wahubiri wapya wanaweza kuhubiri na wahubiri wenye ustadi na uzoefu ili wasaidiwe. Katika maeneo fulani huenda ikawa jambo la hekima kwa wahubiri wawili au zaidi kuhubiri pamoja kwa sababu ya usalama. Hata ikiwa unapanga kuhubiri peke yako katika eneo, kukutana na wengine katika kikundi kunaweza kuwatia moyo. Kujua tu kwamba wengine wanahubiri katika eneo lilelile kunaweza kukupa ujasiri. Mapainia na wengine hawapaswi kuhisi kwamba ni lazima wahudhurie kila mkutano wa utumishi wa shambani uliopangwa na kutaniko, hasa ikiwa mikutano hiyo hufanywa kila siku. Hata hivyo, inaelekea kwamba wanaweza kuunga mkono angalau mikutano kadhaa ya utumishi wa shambani kila juma.
47 Acheni sote tuige mfano uliowekwa na Yesu na mitume wake! Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atabariki jitihada zetu za kushiriki kikamili katika kazi muhimu ya kuhubiri habari njema ya Ufalme.—Luka 9:57-62.
-
-
Njia za Kupanua Huduma YakoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 10
Njia za Kupanua Huduma Yako
YESU alipowaagiza wanafunzi wake wahubiri Ufalme, aliwaambia hivi: “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache.” Kulikuwa na kazi nyingi, basi akaongeza hivi: “Mwombeni Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Mt. 9:37, 38) Yesu aliwapa wanafunzi wake maagizo ya kutimiza huduma yao. Alionyesha umuhimu wa kazi hiyo aliposema: “Hamtamaliza kamwe kuzunguka majiji ya Israeli kabla ya Mwana wa binadamu kufika.”—Mt. 10:23.
2 Leo pia, kuna kazi nyingi ya kufanya katika huduma ya shambani. Lazima habari njema ya Ufalme ihubiriwe kabla ya mwisho kuja, na muda unayoyoma! (Marko 13:10) Kwa kuwa shamba ni ulimwengu, tunakabili hali kama ya Yesu na wanafunzi wake, ingawa kwa kiwango kikubwa zaidi. Idadi yetu ni ndogo ikilinganishwa na mabilioni ya wanadamu ulimwenguni, lakini tuna hakika kwamba Yehova atatusaidia. Habari njema ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni pote, na wakati uliowekwa na Yehova utakapofika, mwisho utakuja. Je, tutatanguliza Ufalme wa Mungu maishani ili tutimize huduma yetu kikamili? Tunaweza kujiwekea malengo gani ya kitheokrasi?
3 Akieleza matakwa ya Yehova kwa watumishi wake waliojiweka wakfu, Yesu alisema: “Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Marko 12:30) Tunapaswa kumtumikia Mungu kwa nafsi yote. Hilo linamaanisha kuwa tunaonyesha kwamba tumejiweka wakfu na tumejitoa kikamili kwa kufanya yote tunayoweza katika utumishi wa Yehova. (2 Tim. 2:15) Kila mmoja wetu anaweza kupanua utumishi wake katika njia mbalimbali ikitegemea hali na uwezo wake. Hebu fikiria baadhi ya njia hizo, na uamue malengo ya kitheokrasi unayoweza kujiwekea unapotimiza huduma yako.
KUWA MHUBIRI WA KUTANIKO
4 Wote wanaokubali kweli wana pendeleo la kutangaza habari njema. Hiyo ndiyo kazi kuu ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Kwa kawaida, mwanafunzi wa Yesu Kristo huanza kuzungumza na wengine kuhusu habari njema mara tu anaposikia ujumbe huo. Hivyo ndivyo Andrea, Filipo, Kornelio, na wengine walivyofanya. (Yoh. 1:40, 41, 43-45; Mdo. 10:1, 2, 24; 16:14, 15, 25-34) Je, inamaanisha kwamba mtu anaweza kuzungumza na wengine kuhusu habari njema kabla hajabatizwa? Ndiyo! Mara tu mtu anapostahili kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa kutanikoni, anaweza kuanza kuhubiri nyumba kwa nyumba. Anaweza pia kushiriki katika sehemu mbalimbali za huduma ikitegemea hali na uwezo wake.
5 Mhubiri anapobatizwa, bila shaka yuko tayari kufanya yote anayoweza ili awasaidie wengine wajifunze habari njema. Wanaume na wanawake wana pendeleo la kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Ni pendeleo kushiriki hata kwa sehemu ndogo katika kuendeleza kazi ya Ufalme wa Mungu. Bila shaka, tukipanua huduma yetu na kufikia mapendeleo zaidi ya utumishi tutakuwa na furaha sana.
KUTUMIKIA KATIKA MAENEO YENYE UHITAJI MKUBWA
6 Huenda eneo la kutaniko lenu huhubiriwa kwa ukawaida na ushahidi mzuri unatolewa. Ikiwa ndivyo, huenda ukahisi kwamba unaweza kupanua huduma yako kwa kuhamia eneo lenye uhitaji mkubwa wa wahubiri. (Mdo. 16:9) Ikiwa unatumikia ukiwa mzee au mtumishi wa huduma, huenda kuna kutaniko lingine ambalo litathamini msaada wako. Mwangalizi wenu wa mzunguko anaweza kukupendekezea jinsi ya kusaidia kutaniko lingine katika mzunguko wenu. Ikiwa ungependa kutumikia katika eneo lingine nchini kwenu, ofisi ya tawi inaweza kukupatia habari zaidi.
7 Je, ungependa kutumikia katika nchi nyingine? Ikiwa ndivyo, unapaswa kufikiria jambo hilo kwa makini. Kwa nini usizungumzie jambo hilo na wazee wa kutaniko lenu? Bila shaka, hilo litakuwa badiliko kubwa kwako na kwa wale watakaoenda nawe. (Luka 14:28) Hata hivyo, ikiwa hukusudii kukaa kwa muda mrefu, huenda ikafaa ufikirie kutumikia katika eneo lililo nchini kwenu.
8 Katika nchi fulani, ndugu wanaosimamia kazi ni wapya katika kweli. Kwa unyenyekevu, ndugu wenyeji wako tayari kuwaachia wazee wenye uzoefu wanaohamia katika makutaniko yao waongoze mambo. Ikiwa wewe ni mzee na unafikiria kuhamia katika nchi kama hizo, kumbuka kwamba lengo lako si kuchukua mapendeleo ya ndugu wenyeji. Badala yake, tumikia pamoja nao. Watie moyo wafanye maendeleo na wakubali majukumu kutanikoni. (1 Tim. 3:1) Uwe na subira ikiwa mambo fulani hayafanywi kama yanavyofanywa katika nchi yenu. Tumia uzoefu wako ukiwa mzee kuwasaidia akina ndugu. Kisha, ikiwa wakati fulani utalazimika kurudi katika nchi yenu, wazee wenyeji watakuwa na uwezo wa kusimamia kutaniko.
9 Kabla ofisi ya tawi haijakupa majina ya makutaniko yanayoweza kufaidika na msaada wako, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko lenu itahitaji kutuma barua ya kukupendekeza. Barua hiyo inahitajiwa hata kama wewe ni mzee, mtumishi wa huduma, painia, au mhubiri. Halmashauri ya utumishi itatuma barua ya kukupendekeza pamoja na ombi lako moja kwa moja kwenye ofisi ya tawi ya nchi unayotaka kutumikia.
KUHUBIRI KATIKA LUGHA NYINGINE
10 Ili upanue huduma yako, huenda ukafikiria kujifunza lugha nyingine, kutia ndani lugha ya alama. Kama una lengo la kujifunza kuhubiri katika lugha nyingine, unaweza kuzungumza na wazee na mwangalizi wa mzunguko. Wanaweza kukupa madokezo na kukutia moyo. Kupitia mwelekezo wa ofisi ya tawi, mizunguko fulani imepanga madarasa ya lugha ili kuwazoeza wahubiri wenye uwezo na mapainia kuhubiri katika lugha nyingine.
UTUMISHI WA PAINIA
11 Wahubiri wote wanapaswa kujua matakwa ya msingi ya utumishi wa painia msaidizi, wa kawaida, na wa pekee na pia utumishi mwingine wa wakati wote. Painia anapaswa kuwa Mkristo aliyebatizwa mwenye mfano
-