-
‘Mungu Ndiye Anayeikuza’!Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
-
-
‘Mungu Ndiye Anayeikuza’!
“Yeye anayepanda si kitu wala yeye anayetia maji, bali Mungu anayeikuza.”—1 KOR. 3:7.
1. Sisi ni “wafanyakazi wenzi wa Mungu” kwa njia gani?
“WAFANYAKAZI wenzi wa Mungu.” Hivyo ndivyo mtume Paulo alivyosema kuhusu kazi ya pekee ambayo sote tunaweza kufanya. (Soma 1 Wakorintho 3:5-9.) Paulo alikuwa akizungumzia kazi ya kufanya wanafunzi. Alilinganisha kazi hiyo na kazi ya kupanda mbegu na kuzitia maji. Tunahitaji msaada wa Yehova ili tufanikiwe katika kazi hiyo ya maana. Paulo anatukumbusha kwamba ‘Mungu ndiye anayeikuza.’
2. Kwa nini ukweli wa kwamba ‘Mungu ndiye anayeikuza’ unatusaidia kuwa na maoni yanayofaa kuhusu huduma yetu?
2 Ukweli huo wenye kunyenyekeza unatusaidia kuwa na maoni yanayofaa kuhusu huduma yetu. Huenda tukahubiri na kufundisha kwa bidii sana, lakini mwishowe Yehova ndiye anayestahili kusifiwa mwanafunzi mpya anapokua kiroho. Kwa nini? Kwa sababu hata tukijitahidi kadiri gani, hakuna yeyote kati yetu anayeweza kuelewa kikamili jinsi mtu anavyokua kiroho, na bila shaka hatuna uwezo wa kuongoza ukuzi huo. Mfalme Sulemani alieleza kwa usahihi jambo hilo alipoandika hivi: “Hujui kazi ya Mungu wa kweli, anayefanya mambo yote.”—Mhu. 11:5.
3. Kazi ya kupanda mbegu halisi inalingana namna gani na kazi ya kufanya wanafunzi?
3 Je, kazi yetu inafadhaisha kwa sababu hatuwezi kuelewa ukuzi wa kiroho? Hapana. Badala yake, hilo linafanya kazi yetu iwe yenye kusisimua na kupendeza. Mfalme Sulemani alisema hivi: “Asubuhi panda mbegu zako na mpaka jioni usiache mkono wako upumzike; kwa maana hujui ni wapi hii itafanikiwa, hapa au pale, au ikiwa zote mbili zitakuwa njema.” (Mhu. 11:6) Kwa kweli, tunapopanda mbegu halisi, hatujui kama itachipuka au mahali itakapochipukia. Kuna mambo mengi kuhusu ukuzi ambayo hatuwezi kuyaongoza. Ndivyo ilivyo na kazi ya kufanya wanafunzi.
-
-
‘Mungu Ndiye Anayeikuza’!Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
-
-
8. (a) Mpandaji anawakilisha nani? (b) Kwa nini watu wanaohubiriwa kuhusu Ufalme wanaitikia kwa njia mbalimbali?
8 Mpandaji anawakilisha nani? Anawakilisha wafanyakazi wenzi wa Mungu, ambao wanatangaza habari njema ya Ufalme. Wanapanda na kutia maji kama Paulo na Apolo walivyofanya. Lakini hata ingawa wanafanya kazi kwa bidii, matokeo wanayopata yanatofautiana. Kwa nini? Kwa sababu ya hali tofauti-tofauti za mioyo ya wale wanaosikiliza ujumbe huo. Katika mfano huo, mpandaji hawezi kamwe kuamua matokeo. Hilo linawafariji kama nini hasa ndugu na dada waaminifu ambao wamehubiri kwa miaka mingi, wengine wao kwa makumi ya miaka, bila kupata matokeo mengi mazuri!a Kwa nini?
9. Mtume Paulo na Yesu walikazia ukweli gani wenye kufariji?
9 Uaminifu wa mpandaji haupimwi kwa matokeo ya kazi yake. Paulo alikazia jambo hilo aliposema hivi: “Kila mtu atapokea thawabu yake mwenyewe kulingana na kazi yake mwenyewe.” (1 Kor. 3:8) Anapokea thawabu kulingana na kazi, si kulingana na matokeo ya kazi hiyo. Vivyo hivyo, Yesu alikazia jambo hilo wanafunzi wake waliporudi kutoka katika safari ya kuhubiri. Walishangilia sana kwa sababu roho waovu walitiishwa kwao kwa jina la Yesu. Hata ingawa habari hizo zilikuwa zenye kusisimua sana, Yesu aliwaambia hivi: “Msishangilie juu ya hili, kwamba roho wanatiishwa kwenu, bali shangilieni kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.” (Luka 10:17-20) Hata mahali ambapo huenda mpandaji haoni ongezeko kubwa kwa sababu ya kazi yake, haimaanishi kwamba hajajitahidi sana au si mwaminifu kama wengine. Kwa kadiri kubwa, matokeo yanategemea hali ya moyo wa msikilizaji. Lakini mwishowe, Mungu ndiye anayeikuza!
-
-
‘Mungu Ndiye Anayeikuza’!Mnara wa Mlinzi—2008 | Julai 15
-
-
a Kwa mfano, fikiria huduma ya Ndugu Georg Fjölnir Lindal huko Iceland iliyosimuliwa katika Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2005, ukurasa wa 210-211, na mambo yaliyoonwa ya watumishi waaminifu ambao walivumilia huko Ireland kwa miaka mingi bila kupata matokeo ya haraka, kama yanavyosimuliwa katika Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 1988, ukurasa wa 82-99, Kiingereza.
-