-
Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika Jumanne, Septemba 2, Ndugu Rutherford alieleza hivi: “Utume wa Mkristo duniani . . . ni kupiga mbiu ya ujumbe wa ufalme wa uadilifu wa Bwana, ambao utaleta baraka kwa uumbaji wote wenye kuugua.” Siku tatu baadaye, Ijumaa, Septemba 5, ambayo iliitwa Siku ya Wafanyakazi Wenzi, Ndugu Rutherford alitaarifu zaidi hivi: “Katika pindi ya fikira nzito kiasili Mkristo hujiuliza hivi, Kwa nini mimi nipo duniani? Na lazima jibu liwe, Kwa neema Bwana amenifanya kuwa balozi nipeleke ujumbe wa kimungu wa ufuniko kwa ulimwengu, na pendeleo na wajibu wangu ni kutangaza ujumbe huo.”
-
-
Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
‘Mtangaze Mfalme na Ufalme’
Katika 1922 Wanafunzi wa Biblia walirudi Cedar Point kwa ajili ya programu ya siku tisa, kuanzia Septemba 5 hadi 13. Msisimko ulikuwa mwingi sana wakati wajumbe walipokuwa wakiwasili kwa ajili ya mkusanyiko huo wa kimataifa. Upeo wa mkusanyiko ulifikiwa Ijumaa, Septemba 8, wakati Ndugu Rutherford alipotoa hotuba “Ule Ufalme.”
Thomas J. Sullivan alikumbuka baadaye hivi: “Wale waliopendelewa kuhudhuria mkutano huo wangali wanaweza kuwazia akilini bidii ya moyo ya Ndugu Rutherford wakati alipowaambia watu wachache wasiotulia ambao walikuwa wakitembea huku na huku kwa sababu ya joto kali ‘WAKETI’ na ‘KUSIKILIZA’ hotuba kwa vyovyote.” Wale waliofanya hivyo hawakukatishwa tamaa, kwa kuwa hiyo ndiyo iliyokuwa hotuba yenye kufanyiza historia ambayo Ndugu Rutherford alihimiza wasikilizaji wake ‘wamtangaze Mfalme na Ufalme.’
Wasikilizaji waliitikia kwa idili kubwa. The Watch Tower liliripoti hivi: “Kila mmoja aliyekuwapo alikazia akilini sana uhakika wa kwamba jukumu liliwekwa juu ya kila mmoja wa wale waliojitakasa kuanzia wakati huo na kuendelea kutenda akiwa wakili wa kutangaza wa Mfalme na ufalme.” Wanafunzi wa Biblia walitoka kwenye mkusanyiko huo wakiwa wanawaka bidii ya kazi ya kuhubiri. Kama vile Dada Ethel Bennecoff, kolpota mmoja ambaye wakati huo alikuwa katika miaka yake ya mwishomwisho ya 20, alisema, “tulichochewa ‘kumtangaza, kumtangaza, kumtangaza Mfalme na ufalme wake’—Naam, kwa bidii na upendo zaidi katika mioyo yetu kuliko ilivyopata kuwa hapo awali.”
-