-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Brazili
Paulo anaishi kwenye shamba la mifugo kaskazini mwa nchi hiyo. Mwanamke aliyeishi naye, na ambaye alimwoa baadaye, alikuwa akijifunza Biblia, kwa hiyo akaamua kujifunza ili tu ampendeze. Wakati huo, wachungaji wa ng’ombe kwenye shamba hilo walifukuza na hatimaye wakamuua chui aliyekuwa akiwaua ng’ombe. Wachungaji hao walitaka kunufaika kutokana na tukio hilo. Hivyo wakampigia simu mwenye shamba hilo na kumwomba pesa za kumlipa mwindaji stadi wa chui. Paulo alikubaliana na njama hiyo, na hata akamwambia mkubwa wake kwamba wachungaji hao walisema kweli. Hata hivyo, dhamiri yake ilimsumbua kwa sababu ya mambo aliyokuwa amejifunza katika Biblia. Alimpigia mkubwa wake simu na kumwambia ukweli, ijapokuwa alijua angeweza kupoteza kazi yake na wafanyakazi wenzake wangekasirika. Baadaye, Paulo alipandishwa cheo akawa msimamizi wa shamba hilo kwa sababu ya unyoofu wake. Sasa Paulo na mke wake ni wahubiri wa habari njema waliobatizwa. Inafurahisha kama nini kumwona mwanamume huyo mnyoofu akiendesha tingatinga lake kuja kwenye Jumba la Ufalme, akiwa amembeba mke wake na watoto wao wawili!
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 58]
Paulo na familia yake
-