Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Estonia
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • NJIA MBALIMBALI ZA KUHUBIRI ISIVYO RASMI

      Ndugu waliokuwa wakitumia lugha ya Kirusi walikuwa wenye bidii na ujasiri na hawakusita kuzungumza na watu katika vikao visivyo rasmi. Kwa mfano, wangeanzisha mazungumzo na watalii ambao walikuwa wakitembelea makanisa huko Tallinn na kuwahubiria. Mara nyingi watalii walifikiri kwamba mtu anayezungumza kuhusu Biblia alikuwa akiongoza watalii, hivyo walisikiliza kwa makini yale ambayo ndugu hao walisema.

      Dada fulani walihubiri katika gari-moshi. Walikuwa wakinunua tiketi iliyowawezesha kusafiri kutoka Tartu kwenda Tallinn, kisha kurudi tena Tartu. Safari hiyo ya saa nane iliwapa nafasi nzuri ya kuanzisha mazungumzo pamoja na abiria na kuwahubiria habari njema.

      Maria Pasechnick, ambaye alihamia Estonia kutoka Kazakhstan anasema hivi: “Nilisali ili nipate funzo la Biblia.” Baada ya kufikiria jambo hilo, aliamua kuwahubiria watu ambao alikuwa akingoja pamoja nao kwa muda mrefu kwenye foleni ndefu, akisubiri kununua chakula katika maduka.

      Maria anaendelea kusema hivi: “Siku moja nilipokuwa nimepanga foleni, nilianza kuzungumza na mwanamke fulani, na hatua kwa hatua nikaanza kuelekeza mazungumzo katika Biblia. Mwanamke huyo hakupendezwa sana, lakini alinipeleka kwa rafiki zake na kunitambulisha kwao, kisha akaniacha niendelee na mazungumzo pamoja nao. Kwa hiyo, niliweza kuanzisha mafunzo manne ya Biblia. Mwanamke mmoja alibatizwa na kuwa Shahidi na anaendelea kumtumikia Yehova kwa uaminifu.”

  • Estonia
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • KUTOA USHAHIDI CHINI YA MARUFUKU

      Lembit Reile, ambaye sasa anatumika katika Halmashauri ya Tawi ya Estonia anasema hivi: “Nilipokuwa shuleni, nilikuwa nikizungumza kwa busara na wengi wa wanafunzi wenzangu. Nilikuwa nikimwalika kijana mmoja nyumbani kwetu, na kumhubiria kwa busara. Baada ya kumaliza shule, sikumwona tena kwa karibu miaka 20. Hivi karibuni, nilipokuwa nikitoa hotuba ya watu wote katika kutaniko la nyumbani kwetu, je, unaweza kukisia ni nani aliyekuwa miongoni mwa wasikilizaji? Ni yule mwanafunzi mwenzangu! Alikuwa akijifunza na Mashahidi wa Yehova, na muda mfupi baada ya ziara yangu katika kutaniko hilo, alibatizwa! Nilifurahi kama nini!”

      Kwa sababu kazi yetu ilikuwa imepigwa marufuku, akina ndugu walihitaji kuwa macho walipohubiri. Mzee mmoja anaeleza jinsi walivyofanya hivyo: “Tulichunguza kwa makini watu waliotuzunguka na ambao tungeweza kuanzisha mazungumzo pamoja nao bila shida. Tulihitaji kuwa na busara sana tulipozungumza na watu tusiowajua. Baada ya muda, mara nyingi tungeweza kutambua ikiwa mtu alikuwa anawapasha habari maofisa wa KGB. Pia, ikiwa mtu alikuwa anazungumza sana au kwa sauti kubwa, tungekuwa na shaka. Kwa upande mwingine, ilikuwa salama kuzungumza na mtu mkimya. Mara nyingi tulianzisha mazungumzo na watu ambao hawakuunga mkono serikali ya Kikomunisti—watu walioitwa waasi, ambao walikuwa tayari kusikiliza maoni ya wengine.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki