-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Bryon anasema: “Sikuzote nimetamani kujifunza Biblia, lakini kila nilipoenda kanisani na marafiki wangu, waliimba nyimbo au kucheza tu.” Bryon aliendelea na masomo yake na riadha. Alijifunza lugha tano na hata akalipiwa masomo ya chuo, lakini hakuridhika kiroho. Kwa hiyo akasali apate kweli.
“Nilitamani sana kupata majibu ya maswali yangu,” Bryon anasema. “Niliamua kutafuta kituo cha Mashahidi wa Yehova kwenye Intaneti kwa sababu Mashahidi fulani tuliokuwa marafiki shuleni waliniambia kwamba jina la Mungu ni Yehova. Nilifungua kituo chao na kuanza kusoma broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Hatimaye, maswali yangu yalijibiwa.” Bryon aliomba funzo la Biblia, akafanya maendeleo haraka, na kujiweka wakfu kwa Yehova mwaka wa 2004. Sasa yeye ni painia wa kawaida na anatumaini kuwa mmishonari aliyepata mazoezi ya Biblia na hivyo kutumia lugha alizojifunza.
-
-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Denise alikuwa na maswali kuhusu imani ya Mashahidi wa Yehova, lakini alisita kwenda kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu na kwao. Badala yake, aliamua kutafuta habari kuhusu Mashahidi kwenye Intaneti, na akapata kituo cha www.watchtower.org. Habari alizopata zilimsadikisha kwamba alikuwa amepata kweli, lakini akasita kuomba funzo la Biblia kwa sababu alijua kuwa atahitaji kubadili maisha yake yapatane na viwango vya Biblia. Alijaza mara nne ile fomu inayojazwa na watu wanaotaka kutembelewa, lakini kila alipoijaza, alishindwa kuituma.
Mnamo Machi (Mwezi wa 3) 2007, Denise alijaza fomu hiyo kwa mara ya tano na wakati huu akatuma ombi lake la kutaka atembelewe. Ombi hilo lilitumwa katika kutaniko lililo karibu na kwao, na wazee wakamwomba dada Vonnie amtembelee. Katika juma la kwanza baada ya Vonnie kumtembelea, Denise alianza kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme.
Kufikia mwisho wa Septemba (Mwezi wa 9), Denise alikuwa ameharibu vitu vyake vya kidini, akakatiza uhusiano wake na dini, na kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa. Yeye na wanawe wawili walifanya maendeleo haraka, na mwana wake mwenye umri wa miaka minane akajiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Denise alibatizwa Januari 2008, na miezi miwili baadaye akawa painia msaidizi. Hayo yalitendeka mwaka mmoja tu baada ya kutuma fomu ya kutaka atembelewe. Denise anasema: “Kama singalifungua kituo hicho cha Intaneti, singalikuwa nikiwaeleza mambo haya.”
-