Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kazi ya Kuhubiri Yenye Kufurahisha Sana
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 15
    • Tangu Oktoba mwaka wa 1996, wahubiri wengine wa habari njema wameombwa kushiriki katika kazi hiyo pamoja na mapainia wa pekee. Wahubiri wa Ufalme na vilevile mapainia wa kawaida wanaotaka kutumikia mahali palipo na uhitaji mkubwa hujiunga na mapainia wa pekee katika sehemu mbalimbali. Wengine wao hutumwa katika makutaniko yaliyo katika maeneo hayo ya pekee ili kuhubiri na kuwasaidia wanaopendezwa. Wahubiri na mapainia wengi wachanga wamekubali mwaliko huo, nao wamejionea mambo mengi yenye kutia moyo.

      Kwa mfano, Abimael, kijana Mkristo aliyekuwa na kazi yenye mshahara mkubwa katika kampuni ya simu za mkononi, aliamua kushiriki katika kazi ya kuhubiri maeneo hayo ya mbali. Waajiri wake walipojua kwamba alitaka kuacha kazi, waliahidi kumpandisha cheo na kumwongezea mshahara. Wafanyakazi wenzake walisisitiza kwamba hiyo ilikuwa nafasi ya pekee na ingekuwa upumbavu kuikataa. Hata hivyo, Abimael alikuwa ameazimia kuunga mkono kazi hiyo ya pekee ya kuhubiri kwa miezi mitatu. Baada ya kufurahia utumishi huo, Abimael ameamua kuendelea kutumikia katika kutaniko la mbali ambapo wahubiri wa Ufalme wanahitajiwa sana. Sasa ana kazi ya mshahara mdogo na amejifunza kufanya maisha yake kuwa sahili.

  • Kazi ya Kuhubiri Yenye Kufurahisha Sana
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 15
    • Wazee Wanashiriki

      Hata hivyo, kazi hii si ya vijana peke yao. Dada mzee, Adela, alikuwa akitamani sana kutumia muda mwingi zaidi katika kazi ya kuhubiri. Alipata nafasi ya kuongeza utumishi wake alipoalikwa kushiriki katika kazi hii ya pekee ya kuhubiri. Anasema hivi: “Nilifurahia sana utumishi wangu hivi kwamba niliwaomba wazee wa kutaniko waniruhusu niendelee kutumikia huko. Ninafurahi kwa sababu ingawa nimezeeka, bado ninaweza kumtumikia Yehova.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki