-
Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Idadi kubwa ya wakazi wa Peru huishi katika vijiji vidogo vilivyotawanyika juu ya milima ya Andes na katika misitu izungukayo vyanzo vya mto Amazon. Wangeweza kufikiwaje? Katika 1971 familia moja ya Mashahidi kutoka Marekani ilisafiri kwenda Peru ili kutembelea mwana wao mishonari, Joe Leydig. Walipopata kujua juu ya ile hesabu kubwa ya vijiji vinavyojificha hapa na pale katika mabonde ya milimani, kuhangaikia watu hao kuliwasukuma watake kufanya jambo fulani ili kusaidia. Walisaidia kuandaa gari moja kwanza ambalo lingetumika kama nyumba, kisha mengine mawili, pamoja na pikipiki ziwezazo kupitia vijia vyembamba ili zitumiwe kufunga safari ndefu za kuhubiri katika maeneo hayo ya mbali.
-
-
Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Jitihada kubwa ilitakwa ili kukusanya watu kama hao wenye mfano wa kondoo kuwa makutaniko na kuwazoeza kushiriki katika utumishi wa Yehova. Kwa kielelezo, katika Argentina, Rosendo Ojeda alisafiri kwa ukawaida kilometa kama 60 kutoka General San Martín, Chaco, ili kuongoza mkutano katika makao ya Alejandro Sozoñiuk, mtu mmoja mwenye kupendezwa. Safari hiyo mara nyingi ilichukua saa kumi, sehemu yayo kwa baiskeli, na nyingine kwa miguu, nyakati nyingine alipitia katikati ya maji yaliyofika makwapani. Mara moja kwa mwezi kwa miaka mitano alifunga safari hiyo, akikaa juma moja kila wakati ili kutoa ushahidi katika eneo hilo. Je, kulistahili? Yeye hana shaka juu ya jambo hilo kwa sababu matokeo yalikuwa kutaniko la wasifaji wa Yehova wenye furaha.
-