Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?
    Amkeni!—2007 | Novemba
    • Philip alikuwa mshiriki wa genge la uhalifu nchini Afrika Kusini. Alizoea kupigana, kuiba, na kutumia lugha chafu. Alifungwa jela kwa sababu ya makosa yake. Ijapokuwa alikuwa akiishi maisha mabaya, Philip alitamani kumjua Mungu. Baada ya kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, alisitawisha tamaa ya kumtumikia Mungu na akaamua kusafisha maisha yake. Aliacha mazoea yake mabaya na akakatisha uhusiano pamoja na rafiki zake wahalifu. Ni kweli gani za Biblia zilizomchochea kufanya mabadiliko hayo?

      Mashahidi wa Yehova walimwonyesha maneno ya Yesu yanayopatikana katika andiko la Yohana 6:44, ambalo linasema hivi: “Hakuna mtu anayeweza kuja kwangu isipokuwa Baba, aliyenituma, amvute.” Philip anasema hivi: “Yehova aliona jambo fulani zuri ndani yangu naye akanivuta kwa watu wake, undugu mzuri kama nini!” Pia, Philip alithamini masimulizi ya Biblia kuhusu huruma za Yehova kuwaelekea watenda-mabaya wanaotubu. Philip anasema hivi: “Masimulizi hayo, yalinisaidia kuona jinsi Yehova alivyo na usawaziko anaposhughulika na wanadamu wasio wakamilifu wanaotubu.”—2 Samweli 12:1-14; Zaburi 51.

  • Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?
    Amkeni!—2007 | Novemba
    • Philip na familia yake, Afrika Kusini

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki