Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Ugumu wa Lugha Mpya

      Kikundi kidogo cha wamishonari waliowasili Martinique katika 1949 walikuwa na maarifa kidogo sana ya Kifaransa, lakini walijua kwamba watu walihitaji ujumbe wa Ufalme. Wakiwa na imani halisi walianza kwenda mlango kwa mlango, wakijaribu kusoma mistari michache ya Biblia au dondoo kutoka kwa kichapo walichokuwa wakitoa. Kwa saburi Kifaransa chao kikawa bora hatua kwa hatua.

  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Edna Waterfall, aliyepewa mgawo Peru, hakusahau upesi nyumba ya kwanza aliyojaribu kutoa ushahidi kwa Kihispania. Huku akitokwa jasho kwa kuona wasiwasi, alijikwaakwaa katika utoaji wake uliokaririwa, akatoa fasihi, na kupanga kuwa na funzo la Biblia pamoja na bibi mzee-mzee. Kisha mwanamke huyo akasema katika Kiingereza safi: “Ni sawa basi. Nitajifunza nawe na tutafanya hivyo katika Kihispania tu ili nikusaidie ujifunze Kihispania.” Akiwa ameshtuka, Edna alijibu: “Wajua Kiingereza? Na uliniacha niseme yote hayo katika Kihispania changu cha jikoni?” “Ilikufaa,” yule mwanamke akajibu. Na, kwa kweli, ilimfaa! Kama vile Edna alivyokuja kuthamini baadaye, hasa kusema katika lugha fulani ni sehemu muhimu ya kujifunza lugha hiyo.

  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kujifunza lugha ya mahali kumekuwa jambo la muhimu katika kupata utumainifu wa watu. Katika maeneo fulani, kuna kutoamini wageni kwa kiasi fulani. Hugh na Carol Cormican wametumikia wakiwa waseja au wakiwa wenzi waliooana katika nchi tano za Afrika. Wanajua vema kuhusu kutoaminiana ambako huwa kati ya Waafrika na watu wa Ulaya. Lakini wanasema: “Kusema katika lugha ya mahali huondoa hisi hizo upesi. Zaidi ya hiyo, wengine ambao hawaelekei kusikiliza habari njema kutoka kwa wananchi wenzao wanakuwa wenye utayari wa kutusikiliza, kuchukua fasihi, na kujifunza, kwa sababu tumefanya jitihada ili kusema nao katika lugha yao wenyewe.” Ili kufanya hivyo, Ndugu Cormican alijifunza lugha tano, mbali na Kiingereza, na Dada Cormican alijifunza sita.

      Bila shaka, kwaweza kuwa na matatizo wakati mtu anapojaribu kujifunza lugha mpya. Katika Puerto Riko ndugu aliyejitolea kucheza kwa kutumia kinanda ujumbe wa Biblia uliorekodiwa kwa wenye nyumba angefunga kinanda chake na kwenda kwenye mlango uliofuata wakati mtu alipojibu, “¡Como no!” Kwake, ilisikika kama “La,” na ilichukua muda kabla hajajua kwamba maneno hayo yalimaanisha “Ndiyo bila shaka!” Kwa upande ule mwingine, wakati mwingine wamishonari hawakuelewa wakati mwenye nyumba aliposema hapendezwi, kwa hiyo waliendelea tu kuhubiri. Kama tokeo, wenye nyumba wachache wenye huruma walinufaika.

      Kulikuwa na hali za kuchekesha pia. Leslie Franks, katika Singapore, alijifunza kwamba ni lazima awe mwangalifu asiseme juu ya nazi (kelapa) alipomaanisha kichwa (kepala), na nyasi (rumput) alipomaanisha nywele (rambut). Mishonari mmoja katika Samoa, kwa sababu ya kutamka vibaya, alimuuliza mwenyeji, “Ndevu zako zikoje?” (yule mwenyeji hakuwa na ndevu), wakati lile lililokusudiwa lilikuwa kuulizia kwa adabu hali ya mke wake. Katika Ekuado, wakati dereva wa basi alipoanza kuendesha basi kwa ghafula, Zola Hoffman, aliyekuwa amesimama ndani ya basi, alitupwa kinyumenyume na kuanguka mapajani mwa mwanamume mmoja. Huku akiona aibu, alijaribu kuomba msamaha. Lakini lile alilosema lilikuwa, “Con su permiso” (Ukiniruhusu). Wakati mwanamume yule kwa ucheshi alipojibu, “Haya basi, endelea kuketi, Bibi,” abiria wale wengine waliangua kicheko.

      Hata hivyo, matokeo mazuri katika huduma yalikuwa yanapatikana kwa sababu wamishonari walijitahidi. Lois Dyer, aliyewasili Japani katika 1950, akumbuka shauri alilopewa na Ndugu Knorr: “Fanya yote uwezayo, na, hata iwapo ukifanya makosa, fanya jambo fulani!” Yeye alifanya hivyo, na ndivyo na wengine wengi. Wakati wa miaka 42 iliyofuata, wamishonari waliotumwa Japani waliona idadi ya wapiga-mbiu wa Ufalme ikiongezeka kutoka wachache tu hadi zaidi ya 170,000 na ukuzi umezidi kuendelea tu. Ni thawabu kubwa jinsi gani kwa sababu, baada ya kumtegemea Yehova ili kupata mwelekezo, walikuwa wenye nia ya kujaribu!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki