-
Maji Yanayobubujika Ili Kutokeza Uzima wa MileleMnara wa Mlinzi—2008 | Juni 1
-
-
Hivi ndivyo kijana mmoja huko Hispania alivyogeuzwa. Alfonso anaeleza hivi: “Nilipokuwa na umri wa miaka 18, maisha yangu hayakunifurahisha.” Alikuwa mraibu wa dawa za kulevya na mhalifu sugu. “Nilijihisi mchafu kwa sababu ya jinsi nilivyoutendea mwili wangu na kuwatendea wengine.
“Shuleni, nilimwona msichana fulani wa rika langu aliyekuwa safi na asiye na hila, jambo lililomfanya awe tofauti kabisa na wanafunzi wengine. Mfano wake ulinifanya nitamani kuishi maisha safi kama yake. Alipendekeza nihudhurie mkutano wa Mashahidi wa Yehova, nami nikahudhuria. Muda si muda nilianza kujifunza Biblia na kusitawisha urafiki pamoja na Mungu. Katika kipindi cha mwaka mmoja, nilisafisha maisha yangu, nikabatizwa na kuwa Shahidi. Mabadiliko hayo makubwa yaliwachochea wazazi wengi katika ujirani wetu kunijia na kuniomba niwasaidie vijana wao waliokuwa waraibu wa dawa za kulevya.”
-
-
Maji Yanayobubujika Ili Kutokeza Uzima wa MileleMnara wa Mlinzi—2008 | Juni 1
-
-
Alfonso, aliyetajwa mapema, amekuja kuthamini sana “maji yaliyo hai” yanayotoka kwa Mungu. Akizungumza kuwahusu wale walioendelea kuishi maisha ya uhalifu na kutumia dawa za kulevya, Alfonso anasema hivi: “Ndugu yangu wa kimwili amekufa, na pia marafiki wangu wote wa zamani. Ujuzi wa Neno la Mungu ulinisaidia kuepuka matokeo hayo mabaya. Niko hai leo kwa sababu ya maandalizi ya kiroho ya Yehova.” Zaidi ya hayo, kwa sababu ya yale ambayo Alfonso amejifunza kutoka kwa Neno la Mungu, anatazamia kuishi milele katika ulimwengu mpya wa Mungu ulioahidiwa.—2 Petro 3:13.
-
-
Maji Yanayobubujika Ili Kutokeza Uzima wa MileleMnara wa Mlinzi—2008 | Juni 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 15]
Alfonso leo, akihubiri Neno la Mungu
-