-
Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?Amkeni!—2007 | Novemba
-
-
Mwanamume Mwaustralia aitwaye Wade alikuwa na zoea la kutumia kileo vibaya na dawa za kulevya, alicheza kamari, na alijihusisha sana katika upotovu wa kingono. Hata hivyo, hakupata furaha. Siku moja alikuwa na mazungumzo na Mashahidi wa Yehova na akakubali kujifunza Biblia. Wade alijifunza nini?
“Nilipendezwa sana na jinsi ambavyo Yesu aliwatendea wengine,” anasema Wade. “Yesu aliwaonyesha fadhili, aliwaonyesha huruma, na kuwapenda watu wote kutia ndani watoto. Kadiri nilivyojifunza ndivyo nilivyotaka kuwa kama yeye. Biblia ilinifundisha jinsi ya kuwa mwanamume halisi na jinsi ya kubadili utu wangu.” Vipi kuhusu matendo yote mabaya aliyofanya? Wade anaendelea kusema hivi: “Biblia ilinifundisha kwamba ikiwa ningetubu dhambi na kubadili mwenendo wangu, Mungu angenisamehe. Kwa kweli, nitaishi milele katika paradiso duniani. Hatimaye nilikuwa na matumaini!” (Mathayo 5:5) Wade alisafisha maisha yake na sasa anamwabudu Yehova akiwa na dhamiri safi.
-
-
Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?Amkeni!—2007 | Novemba
-
-
[Picha katika ukurasa wa 24]
Wade, Australia
-