-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
WENYE MAMLAKA WAHUBIRIWA
Mwaka wa 1938, mwaka mmoja kabla ya Mfalme Zog kupinduliwa, dada zake wawili walienda Boston. Mwezi Desemba gazeti Consolation (ambalo leo huitwa Amkeni!) liliripoti: “Mabinti wa kifalme kutoka Albania walipokuja Boston, mimi na shahidi mwingine kutoka kutaniko la Kialbania la Mashahidi wa Yehova huko Boston, tuliwatembelea hotelini na kuwapa ujumbe wa Ufalme wa Mungu. Walitupokea vizuri.”
Mashahidi hao wawili ni Nicholas Christo na dada yake Lina. Mbali na mabinti wa kifalme walikutana na watu wengine watano wenye vyeo, kutia ndani balozi wa Albania nchini Marekani, Faik Konitza [Konica]. Kabla ya kukutana nao, kikundi hicho kilisomewa kadi ya ushuhuda ya Kialbania inayoeleza jinsi kweli imehubiriwa miongoni mwa Waalbania. Miongoni mwa mambo mengine kadi hiyo ilisema: “Tunafurahi kuwajulisha kwamba ujumbe huu umehubiriwa nchini Albania pia kwa miaka mingi na makumi ya maelfu ya vitabu vimegawanywa kwa wenye mamlaka na watu wa Albania ili kuwapa ujuzi na faraja.”
Balozi Konitza akawaambia mabinti hao wa kifalme: “Wangependa mwasaidie kuhakikisha kwamba kazi yao ya kuhubiri inaendelea bila usumbufu nchini Albania. Dini yao ni ‘mpya,’ na wanaamini kwamba ulimwengu [uliopo sasa] karibuni utakwisha halafu Kristo atatawala kisha hata wafu watafufuliwa.”
Bwana Konitza alipataje kujua mengi hivyo kuhusu ujumbe wa Ufalme? Gazeti Consolation lilieleza kwamba ni “kwa sababu shahidi fulani, kabla ya . . . kujifunza kweli miaka kadhaa awali, alimfahamu vema . . . naye alikuwa amemhubiria mara nyingi.”
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 137]
Nicholas Christo aliwahubiria habari njema watu wenye vyeo vya juu nchini Albania
-