Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?
    Amkeni!—2007 | Novemba
    • Ni Ibada Gani Iliyo Sahihi?

      Angela, msichana Mrumania alipokuwa na umri wa miaka 14, kasisi wa dini ya Pentekoste alimwombea ili apokee roho takatifu, naye akaanza kusema kwa lugha. Lakini wazazi wake walihisi kwamba mafundisho ya dini ya Pentekoste yanapingana na Biblia. Familia yao iliacha kwenda kanisani na ikaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova.

      Ingawa alivunjika moyo mwanzoni, baada ya muda mfupi Angela alianza kuona tofauti kati ya dini yake ya zamani na mafundisho ya Biblia. Kwa mfano, alisoma andiko la Yohana 17:3, ambalo linasema: “Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.” Angela alijifunza kwamba wale wanaopata upendeleo wa Mungu lazima kwanza wawe na ujuzi kumhusu. Angela alijiuliza hivi: “Ningepokeaje roho takatifu ya Mungu kwa njia ya pekee wakati sikuwa naelewa chochote kumhusu?” Anaendelea kusema: “Ninamshukuru Yehova kwa kunisaidia kupata njia inayofaa ya kumwabudu kupitia Neno lake lililoongozwa na roho.”

  • Je, Unaweza Kutegemea Mashauri ya Biblia?
    Amkeni!—2007 | Novemba
    • [Picha katika ukurasa wa 23]

      Angela, Romania

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki