-
Kazi ya Udaktari Itakuwaje Wakati Ujao?Amkeni!—2005 | Januari 22
-
-
‘Nilivutiwa Sana’
Dakt. Jon Schiller, wa Amerika Kaskazini, anasema hivi: “Sawa na watu wengine, nilisomea udaktari ili niwasaidie wagonjwa. Tumaini la kuwa na ulimwengu usio na magonjwa lilinivutia sana. Nilianza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova baada ya kumaliza masomo ya chuoni kuhusu historia ya ustaarabu wa Magharibi. Masomo hayo yalinionyesha kwamba dini zimesababisha matatizo mengi sana na niliona kwamba wanadini walikuwa wakitumia Biblia kwa unafiki. Hivyo nilijiuliza, ‘Biblia inasema nini hasa?’
“Nilipoenda kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova, nilivutiwa kwanza na watu wenye urafiki waliotofautiana sana na wengi wa marafiki wangu. Shahidi mmoja alinijia na kujitolea kunitembelea ili kuzungumza Biblia pamoja nami. Kilichonivutia hasa ni kwamba alinijibu maswali yangu akitumia Biblia.
“Kadiri umri wangu unavyozidi, ndivyo ninavyothamini kwamba mimi ni Shahidi wa Yehova. Mtu anapoanza kufanya kazi ya udaktari yeye hutarajia kutimiza mengi. Lakini mimi huwaona watu wengi ambao wamekata tamaa kwa kutotimiza mengi maishani. Nafikiri jambo bora zaidi katika maisha ya Shahidi wa Yehova ni lile tumaini tulilo nalo la wakati ujao na kuwa na kusudi maishani. Tuwe madaktari, mafundi wa mitambo, au mabawabu, tunajua kwamba tunapomtumikia Mungu sisi hutimiza jambo muhimu sana, kwani sisi humfanyia Yehova kazi fulani. Hilo hutupa uradhi.”
“Kutumia Kanuni za Biblia Kuliboresha Familia Yetu”
Dakt. Krister Renvall, ni daktari huko Ufini, naye hufurahia kuzungumza na watoto. Anasema hivi: “Wakati mmoja nilizungumza na msichana mwenye umri wa miaka 12, ambaye alikuwa akikaribia kufa kutokana na kansa. Msichana huyo alinipa kitabu Amani ya Kweli na Usalama wa Kweli—Kutoka Chanzo Gani?a Nilivutiwa na maelezo yake kuhusu imani yake alipokuwa akikaribia kufa kutokana na ugonjwa huo, lakini sikupata nafasi ya kusoma kitabu alichonipa. Wakati huo nilikuwa na kazi nyingi sana katika kliniki moja huko Helsinki hivi kwamba familia yangu iliathiriwa.
“Hata hivyo, baada ya muda fulani kupita, mke wangu alianza kusoma kitabu hicho. Alisadikishwa mara moja kwamba yale aliyokuwa akisoma ni kweli. Shahidi mmoja wa Yehova alimtembelea na kuanza kujifunza naye Biblia. Mwanzoni, mke wangu aliogopa kunieleza jambo hilo. Lakini aliponieleza, nilimwambia hivi, ‘Ikiwa itasaidia familia yetu, basi ni sawa.’ Nilianza kushiriki katika funzo hilo. Kutumia kanuni za Biblia kuliboresha familia yetu na kubadili maoni yetu kuhusu maisha. Nilifurahi sana kujifunza kuhusu tumaini la ulimwengu usio na magonjwa; sikushangaa kujua kwamba Mungu anakusudia jambo hilo kwa ajili ya wanadamu. Muda mfupi baadaye, mimi na mke wangu tulibatizwa, kisha washiriki wengine wote wa familia wakabatizwa. Ijapokuwa yule msichana mdogo niliyezungumza naye alikufa, imani yake ingalipo.”
-
-
Kazi ya Udaktari Itakuwaje Wakati Ujao?Amkeni!—2005 | Januari 22
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 10, 11]
“NILITAMBUA KWAMBA MAISHA YANA KUSUDI”
“Nilipokuwa nikiwahudumia wanafunzi walemavu, nilitambua kwamba wazazi ambao ni Mashahidi wa Yehova ni tofauti. Ilionekana kwamba waliwashughulikia vizuri zaidi watoto wao walemavu kuliko wazazi wengine. Pia nilitambua kwamba wana elimu bora ikilinganishwa na kazi wanazofanya. Imani yao ilinivutia. Imani yangu ilikuwa imedhoofishwa sana na walimu wa nadharia ya mageuzi. Hata hivyo, masomo yangu ya tiba yalikuwa yamenifanya nistaajabie sana maajabu ya uhai.
“Wakati huohuo, nilitambua kwamba sijui kuwalea watoto wangu. Sikujua mipaka ninayopaswa kuwawekea, mambo ninayopaswa kuwachochea wafanye, au jinsi ya kufanya maisha yao yawe na kusudi. Pia, maisha yangu hayakuwa na kusudi. Nilisali ili kupata msaada.
“Wakati huo, Mashahidi wa Yehova waliniletea gazeti linalozungumzia jinsi ya kuwarekebisha na kuwatia watoto nidhamu kwa upendo. Kanuni za Biblia zilizoelezwa katika gazeti hilo zilinisaidia sana, kwa hiyo nilikubali kujifunza Biblia pamoja nao. Nilipojifunza sababu iliyomfanya Yehova aanzishe uhai na umuhimu wa kifo cha Yesu, nilitambua kwamba maisha yana kusudi. (Yohana 3:16; Waroma 5:12, 18, 19) Nilikuwa nimepotoshwa na nadharia ya mageuzi. Nilifarijika nilipojifunza kwamba Mungu hakukusudia wanadamu wawe wagonjwa na wafe! Sasa ninapata uradhi ninapowafundisha watu wanyoofu jinsi Mungu atakavyoponya magonjwa yote hivi karibuni.”
[Picha]
Helena Bouwhuis alikuwa akiwatibu wanafunzi wa shule huko Uholanzi
-