-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Fiji
Matthew ni mzee wa kutaniko na mmishonari aliyehudhuria Shule ya Gileadi, naye hujifunza na wanafunzi wanne kwenye chuo fulani cha ualimu kila juma. Katika chuo hicho makasisi wa dini mbalimbali huwahubiria waumini wa dini zao jioni. Kusudi la mpango huo ni kuwasaidia wakuu wa chuo hicho kupambana na mwenendo mbaya ambao umeenea chuoni.
Jioni moja, Matthew aliona wanafunzi wengi—wapatao 250—wakiwa wameketi kimya kwenye chumba cha kulia wakiwa na Biblia, vitabu vya kuandikia, na kalamu. Walikuwa wakimngojea kasisi wa madhehebu fulani kubwa ambaye alikuwa aongoze ibada. Lakini kasisi huyo hakufika, kwa hiyo Matthew akaombwa awahutubie. Badala ya nyimbo na hotuba kali ambazo wengine walikuwa wakitoa, Matthew alitoa hotuba tofauti sana akitumia Maandiko. Katika hotuba hiyo ambayo hakuwa ameitayarisha, Matthew aliwatia moyo wanafunzi wamkumbuke Muumba wao wakiwa vijana. Baadaye wanafunzi wote walipanga mstari kumsalimu Matthew kwa mkono na kumshukuru. Sasa anatarajia kwa hamu kuwasaidia wale waliochochewa na hotuba hiyo kutaka kujua zaidi.
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 63]
Matthew
-