-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Japani: “Japani imekumbwa na vimbunga vingi zaidi [katika 2004] kuliko katika mwaka mwingine tangu ilipoanza kurekodi matukio hayo mnamo 1551,” inasema ripoti fulani. Katika wilaya za Niigata na Fukui, hali mbaya ya hewa katika mwezi wa Julai iliharibu nyumba na majengo mengine zaidi ya 34,000, kutia ndani Jumba la Ufalme na nyumba 60 za akina ndugu. Mamia ya ndugu wa makutaniko jirani walitoa msaada bila kukawia. Majuma mawili baadaye, hilo Jumba la Ufalme lilikuwa limerekebishwa kabisa.
Akina ndugu walisaidia pia kusafisha nyumba za watu ambao si Mashahidi wa Yehova wanaoishi karibu na Jumba la Ufalme, na pia kuzipiga dawa za kuua viini. Mtu fulani aliyekuwa akipinga ujumbe wa Ufalme alitokwa na machozi ya furaha. Wenye mamlaka waliiandikia halmashauri ya kutoa misaada ili kuwashukuru akina ndugu kwa kazi yao.
Mnamo Septemba na Oktoba, vimbunga viwili viliikumba Japani, na ndugu mmoja na dada mmoja wakafa katika mafuriko na maporomoko ya udongo. Mashahidi wengine 100 waliathiriwa pia. Jiji la Toyooka, katika Wilaya ya Hyogo lilikumbwa na mafuriko. Mwangalizi wa mzunguko alisaidia kufanya mipango ya kutoa misaada ijapokuwa nyumba yake ilikuwa imejaa maji.
Baada ya maji yenye matope kupungua katika nyumba ambayo dada fulani painia alikuwa amekodi, akina ndugu waliisafisha hadi ikatakata. Mwenye nyumba hiyo si Shahidi, lakini alivutiwa sana. Dada huyo alisema: “Nimekuwa tu nikisikia kuhusu misaada inayotolewa na tengenezo la Yehova, lakini wakati huu mimi binafsi nimesaidiwa. Najivunia pendeleo la kumtumikia Mungu wetu, Yehova, na la kuwa sehemu ya tengenezo lake.”
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 20]
Ndugu wakisafisha Jumba la Ufalme lililoharibiwa na mafuriko katika Wilaya ya Niigata, Japani
-