Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mvua Hainyeshi Kamwe Huku Lima”
    Amkeni!—2003 | Mei 22
    • Mvua Inaponyesha

      Hata hivyo, nyakati nyingine mvua hunyesha kwenye sehemu fulani za jangwa hilo, na pia katika jiji la Lima. Kila baada ya miaka michache, Mkondo baridi wa Peru hutokeza maji yenye joto. Maji hayo hutoka magharibi mwa Bahari ya Pasifiki. Tukio hilo huitwa El Niño, nalo huonyesha kwamba mvua iko karibu. Mvua kubwa ya El Niño ilinyesha hasa katika mwaka wa 1925, 1983, na 1997/1998. Ama kwa hakika, wakaaji wa jangwa hilo, ambao hawajazoea kupata mvua hata kidogo, huwa hawajajitayarishia mvua hiyo kubwa na mafuriko yanayosababishwa nayo.

      Kwa mfano, jiji la Ica huko Peru, lilikumbwa na mafuriko katika mwaka wa 1998. Mto Ica ulifurika na maji hayo yakasambaa katika sehemu nyingi za jiji hilo na kufagia nyumba za matofali. Maeneo mengine ya jangwa hilo yalifaidika kutokana na maji hayo na mimea ikasitawi. Mvua ya El Niño ya hivi karibuni ilifanya maua maridadi na mimea ya kijani isitawi katika Jangwa la Sechura, na hilo linatukumbusha ahadi ya Mungu kwamba siku moja ‘jangwa litachanua maua kama waridi.’ (Isaya 35:1) Mvua hiyo kubwa ilifanyiza pia ziwa kubwa katikati ya jangwa hilo. Inakadiriwa kwamba ziwa hilo lina urefu wa kilometa 300 na upana wa kilometa 40. Magazeti yaliliita ziwa hilo La Niña.

  • “Mvua Hainyeshi Kamwe Huku Lima”
    Amkeni!—2003 | Mei 22
    • [Picha katika ukurasa wa 26]

      Mvua kubwa za El Niño zilisababisha mafuriko makubwa huko Ica, Peru, mnamo Januari 30, 1998

      [Hisani]

      AP Photo/Martin Mejia

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki