-
Kuchagua Mlo Wenye AfyaAmkeni!—1997 | Juni 22
-
-
Piramidi ya Mwongozo wa Chakula
Chagua kwa hekima vyakula zaidi kutoka sehemu za chini za Piramidi ya Mwongozo wa Chakula
Mafuta, oili, na vitu vitamu-vitamu
Tumia kwa uchache
Kikundi cha maziwa, mtindi, Kikundi cha nyama, kuku,
na jibini samaki, maharagwe makavu,
Viasi vya chakula 2-3 mayai, na aina za njugu
kwa siku Viasi vya chakula 2-3 kwa siku
Kikundi cha mboga Kikundi cha matunda
Viasi vya chakula 3-5 kwa siku Viasi vya chakula 6-11 kwa siku
Kikundi cha mkate, chakula cha nafaka, wali, na pasta
Viasi vya chakula 2-4 kwa siku
-
-
Kuchagua Mlo Wenye AfyaAmkeni!—1997 | Juni 22
-
-
Msingi wa Ulaji Wenye Afya
Msingi wa ulaji wenye afya ni kufanya tu machaguo mazuri kutoka kwa vyakula vilivyopo. Kwa msaada wa kufanya machaguo ya kiafya, Idara ya Kilimo ya Marekani hudokeza utumizi wa piramidi yenye safu nne ya mwongozo wa chakula.—Ona chati kwenye ukurasa wa 12.
Chini ya piramidi hiyo kuna kabohaidreti tata, ambazo hutia ndani vyakula vya nafaka, kama vile mkate, chakula cha nafaka, wali, na pasta. Vyakula hivi ndivyo msingi wa ulaji wenye afya. Kwenye safu ya pili kuna sehemu mbili zilizo sawa; moja ni mboga na ile nyingine ni matunda. Vyakula hivi pia ni kabohaidreti tata. Sehemu kubwa ya mlo wako wa kila siku yapaswa kuteuliwa kutoka vikundi hivi vitatu vya chakula.
Safu ya tatu ina sehemu mbili ndogo. Sehemu moja ina vyakula kama vile maziwa, mtindi, na jibini; na ile nyingine hutia ndani nyama, kuku, samaki, maharagwe makavu, mayai, na njugu.a Ni viwango vya kiasi tu vipaswavyo kuliwa kutoka katika vikundi hivi. Kwa nini? Kwa sababu vingi vya vyakula hivi vimejaa kolesteroli na mafuta kifu, ambayo huongeza uwezekano wa hatari ya kupatwa na maradhi ya ateri za moyo na kansa.
Mwishowe, juu kabisa ya piramidi kuna eneo dogo ambalo hutia ndani mafuta, oili, na vitu vitamu-vitamu. Vyakula hivi huandaa virutubisho vichache sana na vyapasa kuliwa kwa uchache sana. Vyakula vingi zaidi vyapasa kuchaguliwa kutoka sehemu ya chini ya piramidi, na vichache kutoka sehemu ya juu.
Badala ya kula tu vyakula vilevile kutoka kila sehemu kuelekea chini ya piramidi, ni jambo la hekima kujaribu vyakula tofauti-tofauti katika sehemu hizo. Hiyo ni kwa sababu kila chakula kina mchanganyiko tofauti wa virutubisho na utembo. Kwa kielelezo, mboga fulani na matunda ni vyanzo vizuri vya vitamini A na C, ilhali nyingine zimejaa asidi jani, kalsiamu, na madini nyingi.
-