-
Vyakula Bora Unavyoweza KupataAmkeni!—2002 | Mei 8
-
-
Watu fulani hugawanya chakula katika vikundi vitatu vikubwa. Kikundi cha kwanza kinatia ndani nafaka, kama vile mahindi, ngano, mchele, oat, shayiri, rai, na mtama, pia viazi, kama vile viazi ulaya na viazi vikuu. Vyakula hivyo vya wanga huongeza nishati mwilini. Kikundi cha pili kinatia ndani aina za maharagwe kama vile soya, dengu, chick-peas, na broad beans na vyakula vingine vinavyotokana na wanyama, kama nyama, samaki, mayai, maziwa, na vyakula vinavyotengenezwa kwa maziwa. Vyakula hivyo vina protini, madini ya chuma, zinki, na vitamini kadhaa. Kikundi cha tatu kinatia ndani matunda na mboga. Vyakula hivyo vina vitamini na madini muhimu. Pia, vinasaidia mwili kupata nyuzinyuzi na nishati, na ni vyanzo pekee vya vitamini C.
-
-
Vyakula Bora Unavyoweza KupataAmkeni!—2002 | Mei 8
-
-
[Picha katika ukurasa wa 26]
KIKUNDI CHA KWANZA: nafaka na viazi
[Picha katika ukurasa wa 26]
KIKUNDI CHA PILI: aina za maharagwe, nyama, samaki, mayai, maziwa, na vyakula vinavyotengenezwa kwa maziwa
[Picha katika ukurasa wa 26]
KIKUNDI CHA TATU: matunda na mboga
-