-
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na kinywa kinachosema mambo makubwa na makufuru akapewa [huyo hayawani mwenye vichwa saba], na mamlaka ya kutenda kwa miezi arobaini na miwili akapewa.
-
-
Kupambana na Hayawani Wawili Wakali SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
22. (a) Ile miezi 42 inarejezea kipindi gani cha wakati? (b) Wakati wa miezi 42, Wakristo wapakwa-mafuta ‘walishindwaje’?
22 Miezi 42 inayotajwa hapa inaonekana kuwa kipindi kile kile cha miaka mitatu na nusu ambacho katika hicho wale watakatifu wanasumbuliwa na ule upembe uliozuka katika mmoja wa wale hayawani katika unabii wa Danieli. (Danieli 7:23-25; ona pia Ufunuo 11:1-4.) Hivyo, kufikia mwishoni mwa 1914 kuendelea mpaka ndani ya 1918, wakati mataifa yenye kupigana yalipokuwa yakiraruana kihalisi kama hayawani-mwitu, wananchi wa mataifa hayo walibanwa wamwabudu hayawani-mwitu, washiriki dini ya utukuzo wa taifa, hata kuwa tayari kufia nchi yao. Mbano kama huo uliongoza kwenye mateso makali upande wa wengi wa wapakwa-mafuta ambao walihisi kwamba utii wao wa juu zaidi ulikuwa wa Yehova Mungu na Mwana wake, Kristo Yesu. (Matendo 5:29) Majaribu yao yalifikia upeo katika Juni 1918, wakati wao ‘waliposhindwa.’ Katika United States, maofisa mashuhuri na wawakilishi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi walitiwa gerezani kimakosa, na kazi ya kuhubiri iliyopangwa kitengenezo ya ndugu zao Wakristo ilizuiwa sana. Akiwa na mamlaka “juu ya kila kabila na kikundi cha watu na ulimi na taifa,” hayawani-mwitu alizuia sana kazi ya Mungu ulimwenguni pote.
-