-
Ukristo Ukitenda Katikati ya MsukosukoMnara wa Mlinzi—1998 | Januari 15
-
-
Watu Watoa kwa Ukarimu
Ndugu katika Ulaya walikuwa na hamu tena ya kusaidia. Ofisi ya Mashahidi wa Yehova katika Louviers, Ufaransa, ilitoa mwito huo katika makutaniko huko Rhône Valley, na pia katika Normandy, na sehemu za eneo la Paris. Hapo kanuni nyingine ya Kimaandiko ilitumika: “Yeye apandaye kwa uhaba atavuna pia kwa uhaba; na yeye apandaye kwa wingi atavuna pia kwa wingi. Acheni kila mmoja afanye kama vile ameazimia moyoni mwake, si kwa kinyongo au kwa shurutisho, kwa maana Mungu hupenda mpaji mchangamfu.”—2 Wakorintho 9:6, 7.
Maelfu ya watu walichukua kwa shangwe hiyo fursa ya kutoa. Masanduku na mifuko ya nguo, viatu, na vitu vingine vilimiminika kwenye Majumba ya Ufalme kisha vikasafirishwa hadi ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika Ufaransa. Huko wajitoleaji 400 walikuwa tayari kushiriki katika hatua iliyofuata ya kampeni ya “Help Zaire” (“Isaidie Zaire”). Bidhaa zilizochangwa zilipomiminika, wajitoleaji hao walitenganisha, kukunja, na kupakia hayo mavazi katika masanduku yaliyorundikwa thelathini-thelathini katika bao la kubebea mizigo. Watoto walikuwa wamefikiria ndugu na dada zao wachanga katika Afrika na walikuwa wamepeleka vichezeo—vigari vyenye kumetameta, pia, wanasesere, na wanasesere wa dubu. Hivyo vilipakiwa pamoja na mahitaji ya lazima ya maisha. Kwa ujumla, masanduku tisa ya meta 12 yalijazwa na kupelekwa Kongo.
Ni msaada kiasi gani ambao umepelekwa Afrika ya Kati kwa msaada wa maelfu ya Mashahidi katika Ubelgiji, Ufaransa, na Uswisi? Kufikia Juni 1997 jumla ya kiasi ilikuwa kilogramu 500 za dawa, tani 10 za biskuti zenye kiwango cha juu cha protini, tani 20 za vyakula vingine, tani 90 za mavazi, jozi 18,500 za viatu, na mablanketi 1,000. Fasihi za Biblia pia zilipelekwa huko kwa ndege. Yote hayo yalithaminiwa sana, yakiwafariji wakimbizi na kuwasaidia ili wavumilie majaribu yao. Gharama ya ugavi ilijumlika kuwa karibu dola 1,000,000 za Marekani. Michango hiyo ilikuwa uthibitisho wenye nguvu wa udugu na upendo miongoni mwa wamtumikiao Yehova.
Ugawanyaji Katika Kongo
Bidhaa zilipoanza kufika Kongo, ndugu wawili na dada mmoja walikuja kutoka Ufaransa ili kufanya kazi na halmashauri za kutoa msaada za huko. Kuhusu shukrani zilizoonyeshwa na Mashahidi wa Kongo, Joseline alisema hivi: “Tulipokea barua nyingi za kuonyesha uthamini. Dada mmoja maskini alinipa kipambo cha malakiti. Wengine walitupatia picha zao wenyewe. Tulipokuwa tukiondoka, dada walinibusu, kunikumbatia, na kutoa machozi. Nilitoa machozi pia. Wengi walitoa maelezo kama vile, ‘Yehova ni mwema. Yehova hutufikiria.’ Kwa hiyo wao watambua kwamba Mungu astahili kusifiwa kwa ajili ya utoaji huo. Tulipokuwa tukigawanya chakula, ndugu na dada walimsifu Yehova kwa nyimbo za Ufalme. Lilikuwa jambo lenye kutia huruma sana.”
Daktari wa kitiba aitwaye Loic alikuwa mshiriki wa kikoa hicho. Wengi walimiminika ndani ya Jumba la Ufalme na kungojea kwa subira zamu yao ya kupata msaada wake. Akitaka kufanya jambo fulani pia, dada mmoja Mkongo alitayarisha na kuchanga maandazi 40 kwa ajili ya wale waliokuwa wakingojea kumwona daktari. Kwa kuwa watu wapatao 80 walikuwa wakingojea, kila mmoja wao alipokea andazi nusu.
-
-
Ukristo Ukitenda Katikati ya MsukosukoMnara wa Mlinzi—1998 | Januari 15
-
-
Upendo wa Kikristo Wadhihirishwa
Miongoni mwa walioshiriki kwa hamu katika mradi wa “Help Zaire” katika Ufaransa alikuwa Ruth Danner. Akiwa mtoto, alitiwa gerezani katika kambi ya mateso ya Nazi kwa sababu ya imani yake ya Kikristo. Alieleza hivi: “Tulikuwa wenye furaha sana kufanya jambo fulani kwa ajili ya ndugu na dada zetu katika Afrika! Lakini kuna kitu kilichonifanya niwe na furaha maradufu. Mwaka wa 1945, tuliporudi nyumbani kutoka Ujerumani, hatukuwa na chochote. Hata mavazi tuliyovaa yalikuwa ya kuazimwa. Ingawa hivyo, upesi tulipokea msaada wa kimwili kutoka kwa ndugu zetu katika Amerika. Kwa hiyo jitihada ya kutoa msaada iliniwezesha kuonyesha fadhili tulizoonyeshwa muda mrefu uliopita. Ni pendeleo lililoje kuwa sehemu ya familia kubwa ya ndugu wanaodhihirisha upendo wa Kikristo!”—Yohana 13:34, 35.
-