-
Kusoma Biblia Kumenitia Nguvu Katika Maisha Yangu YoteMnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 15
-
-
Kipindi cha watalii kilipofika, mimi na painia mwenzangu, Simon Apolinarski, tulilazimika kutafuta mahali pengine pa kuishi, lakini tulikuwa tumeazimia kubaki katika mgawo wetu. Tuliruhusiwa kuishi katika nyumba iliyozeeka ya farasi, ambamo tulilala kwenye magodoro yaliyotengenezwa kwa nyasi zilizokaushwa. Tulihubiri wakati wa mchana. Tulimhubiria mwenye ile nyumba ya farasi, akawa mmoja kati ya watu wengi waliokubali kweli. Baada ya muda mfupi, gazeti la eneo hilo lilichapisha habari ambayo iliwaonya wakaaji wa Dunkerque kuhusu “kuenea kwa kazi ya Mashahidi wa Yehova katika eneo hilo.” Hata hivyo, mimi, Simon, na wahubiri wachache tu ndio tuliokuwa Mashahidi katika eneo hilo! Tulipopata magumu, tulitiwa moyo kwa kutafakari kuhusu tumaini letu la Kikristo na kufikiria jinsi Yehova alivyokuwa ametutunza. Kulikuwa na wahubiri 30 wa kawaida huko Dunkerque nilipopokea mgawo mwingine mwaka wa 1952.
-
-
Kusoma Biblia Kumenitia Nguvu Katika Maisha Yangu YoteMnara wa Mlinzi—2011 | Septemba 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 5]
Mimi na Simon
-