-
Vita vya Kidini Katika UfaransaAmkeni!—1997 | Aprili 22
-
-
Wawaldensi walipata mshindo kamili wa upinzani rasmi. Wao walikuwa kikundi cha watu wachache waliokaza fikira kwenye Biblia ambao waliishi katika vijiji maskini kusini-mashariki mwa nchi hiyo. Wengine walichomwa kwenye miti ya mateso, mamia yakachinjwa, na vijiji 20 hivi vikaangamizwa.—Ona sanduku kwenye ukurasa wa 6.
-
-
Vita vya Kidini Katika UfaransaAmkeni!—1997 | Aprili 22
-
-
Wawaldense Walisimama Imara—Kukiwa na Tokeo Gani?
PIERRE VALDES, au Peter Waldo, alikuwa mfanya-biashara tajiri katika Ufaransa ya karne ya 12. Katika wakati huo ambapo Kanisa Katoliki la Kiroma lilizuia kimakusudi watu kujua Biblia, Waldo aligharimia kutafsiriwa kwa Gospeli na vitabu vingine vya Biblia katika lugha za kawaida za watu wa kusini-mashariki mwa Ufaransa. Kisha akaacha biashara yake na kujitoa kuhubiri Gospeli. Muda si muda wengi walijiunga naye, na katika 1184 yeye na washirika wake walitengwa na ushirika na Papa Lucius wa 3.
Baada ya muda, vikundi hivi vya wahubiri wenye kuelekezea Biblia fikira vikaja kuitwa Wawaldense. Wao walitetea kurudia itikadi na mazoea ya Ukristo wa mapema. Walikataa mazoea na itikadi za kidesturi za Kikatoliki, kutia ndani kuondolewa kwa adhabu ya purgatori, sala kwa wafu, purgatori, ibada ya Maria, kusali kwa “watakatifu,” kubatiza vitoto vichanga, kuheshimu kisalaba, na badiliko la kimuujiza. Likiwa tokeo, Wawaldense mara nyingi waliteseka sana mikononi mwa Kanisa Katoliki. Mwanahistoria Will Durant afafanua hali hiyo wakati Mfalme Francis wa 1 alipoanzisha kampeni dhidi ya watu wasio Wakatoliki:
“Kadinali de Tournon, akidai kwamba Wawaldense walikuwa na njama ya kupindua serikali, alimshawishi Mfalme mgonjwa mwenye kusitasita atie sahihi agizo (Januari 1, 1545) kwamba Wawaldense wote waliopatikana na hatia ya kuasi mafundisho ya kidini wauawe. . . . Kwa kipindi cha juma moja (Aprili 12-18) vijiji kadhaa viliteketezwa kabisa; katika kimoja wanaume, wanawake, na watoto 800 walichinjwa; katika miezi miwili 3,000 waliuawa, vijiji 22 kuteketezwa, na wanaume 700 wakapelekwa kwenye merikebu za kwenda vitani. Wanawake 25 waliopigwa na hofu, wakitafuta kimbilio uvunguni mwa ardhi, walisongwa pumzi kwa kukosa oksijeni kwa sababu ya moto uliowashwa kwenye kiingilio.”
Kuhusu matukio kama hayo ya kihistoria, Durant alisema hivi: “Minyanyaso hii ndiyo iliyokuwa kutofaulu kabisa kwa utawala wa akina Francis.” Lakini hilo lilikuwa na matokeo gani kwa wale waliotazama uthabiti wa Wawaldense wakati wa minyanyaso iliyoamriwa na mfalme? Durant aliandika: “Moyo mkuu wa wafia-imani hao ulipatia mwendo wao adhama na fahari; ni lazima maelfu ya watazamaji yalipendezwa na kusumbuliwa, ambayo bila hukumu hizo zenye kutazamisha, huenda hayangeshughulika kamwe kubadili imani yao iliyorithiwa.”
-