-
Uhuru wa Kusema Je, Unatumiwa Vibaya?Amkeni!—1996 | Julai 22
-
-
Uhuru wa kusema ni mada ya ubishi mwingi sana wakati huu katika Ufaransa. “Bila shaka lolote,” akaandika mtungaji wa vitabu Mfaransa Jean Morange katika kitabu chake juu ya uhuru wa kusema, “historia ya uhuru wa kusema haijakwisha, nayo itaendelea kusababisha migawanyiko. . . . Karibu kila mwaka kuna kutolewa kwa filamu au kipindi cha televisheni au kampeni ya utangazaji isababishayo itikio kali, lenye kuamsha upya mjadala wa kale usiokwisha kuhusu uchujaji.”
Makala moja iliyokuwa katika gazeti la habari la Paris Le Figaro iliripoti kwamba kikundi cha rapu kitwacho Ministère amer (Huduma Chungu) kinahimiza mashabiki wacho kuua polisi. Mojapo mafungu ya maneno yao husema: “Hakutakuwako na amani isipokuwa [polisi] wafe.” “Kwenye muziki wetu,” akatangaza msemaji wa hicho kikundi, “twawaambia wachome vituo vya polisi na kutoa dhabihu [polisi]. Ni nini kingekuwa cha kawaida zaidi ya hicho?” Hakuna hatua yoyote ambayo imechukuliwa dhidi ya kikundi hicho cha rapu.
-
-
Uhuru wa Kusema Nyumbani—Je, Ni Hali Itishayo Kutokeza Matatizo?Amkeni!—1996 | Julai 22
-
-
Kwa kielelezo, katika Ufaransa, wakati wanamuziki wa rapu walipopendekeza uuaji wa polisi na polisi wakauawa na watu fulani waliosikia huo muziki, je, wanamuziki hao wa rapu wangetozwa hesabu kwa kuchochea jeuri? Au wanapaswa kulindwa chini ya mswada wa haki?
-