Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Acha Yehova Akuongoze Kupata Uhuru wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • Kisha akaongezea hivi: “Uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Rom. 8:19-21) “Uumbaji” unarejelea wanadamu ambao wana tumaini la kuishi milele duniani, wale ambao watafaidika wakati wa “kufunuliwa” kwa wana wa Mungu waliotiwa mafuta kwa roho.

  • Acha Yehova Akuongoze Kupata Uhuru wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • 18. Uhuru utaongezekaje kwa wanadamu watiifu, na ni uhuru gani ambao watafurahia mwishowe?

      18 Wakati huo, wanadamu waliokombolewa watapata uhuru mpya kabisa, uhuru kutokana na uvutano wa Shetani na roho waovu. (Ufu. 20:1-3) Jambo hilo litaleta kitulizo kama nini! Kisha, wale 144,000 ambao watakuwa wafalme na makuhani pamoja na Kristo wataendelea kutumia faida za dhabihu ya fidia kuwaweka wanadamu huru hatua kwa hatua mpaka dhambi na hali ya kutokamilika iliyosababishwa na Adamu itakapokuwa imeondolewa kabisa. (Ufu. 5:9, 10) Baada ya kubaki waaminifu hata chini ya jaribu, wanadamu watakuwa wamepata uhuru kamili ambao Yehova alikusudia wawe nao, “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” Hebu fikiria jambo hilo! Hutahitaji tena kupambana na mwili wako ili kufanya mambo yanayofaa machoni pa Mungu kwa sababu mwili wako wote utakuwa mkamilifu na utu wako utakuwa umebadilika kabisa kulingana na utu wa Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki