Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tahiti
    2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mnamo mwaka wa 1969, Ato Lacour pamoja na familia yake walihamia Rurutu, kimojawapo cha Visiwa vya Tubuaï. Tayari alikuwa ameomba ahamishiwe huko kikazi. Alikuwa amebatizwa kwa miaka mitatu tu na hakuna mtu mwingine katika familia yake aliyekuwa Shahidi. Hakukuwa na wahubiri wengine kwenye visiwa hivyo. Siku moja baada ya kufika, alianza kuhubiri. Aliandika hivi katika kitabu chake cha kumbukumbu: “Nimeanza kuhubiri, mimi peke yangu. Si rahisi. Babiloni Mkubwa ametia mizizi kabisa hapa.”

      Hata hivyo, baada ya muda mfupi watu waliopendezwa walianza kukubali habari njema, na kikundi kikaanzishwa. Mwanzoni, walifanya mikutano katika nyumba ya Lacour. Ato anasema hivi: “Kwa kuwa dini yetu ilikuwa mpya kwenye kisiwa hicho, kikundi chetu kilibandikwa jina ‘dini ya Lacour.’ Lakini Yehova ‘aliendelea kukikuza’ kikundi chetu, nacho kikawa kutaniko mwaka wa 1976.” (1 Kor. 3:6)

  • Tahiti
    2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Rudolphe na Narcisse Haamarurai walihamia Bora Bora. Rudolphe, aliyekuwa msimamizi wa kampuni ya umeme katika eneo fulani la Tahiti, aliacha kazi hiyo na akapata kazi ya kuchuma na kukausha nazi huko Bora Bora. Hakupata kazi nyingine kwa miaka miwili. Lakini Yehova alimbariki sana yeye na mkewe, kwa kuwa hatimaye kutaniko lilianzishwa kwenye kisiwa hicho! Kutaniko hilo lilifanya mikutano nyumbani kwa Ndugu Haamarurai kwa zaidi ya miaka 25. Kisha, katika mwaka wa 2000, wakaanza kutumia Jumba lao jipya la Ufalme lililo karibu na kidimbwi maridadi cha Bora Bora.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki