-
Upole Ni Sifa Muhimu Sana ya KikristoMnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 1
-
-
Huenda zamani tulizoea kuzungumza kwa ukali na kutenda bila huruma. Hata hivyo baada ya kujifunza kweli ya Biblia, tulibadilika tukawa na utu wenye kupendeza. Paulo alizungumzia badiliko hilo alipowahimiza Wakristo wenzake hivi: “Jivikeni wenyewe shauku nyororo za huruma, fadhili, hali ya akili ya kujishusha chini, upole, na ustahimilivu.” (Wakolosai 3:12) Biblia inafananisha badiliko hilo na jinsi wanyama wakali wa mwituni kama mbwa-mwitu, chui, simba, dubu, na nyoka wanavyobadilika na kuwa kama wanyama wapole wa kufugwa kama vile mwana-kondoo, mwana-mbuzi, ndama, na ng’ombe. (Isaya 11:6-9; 65:25) Mabadiliko hayo huwa ya kipekee sana hivi kwamba wengine hushangaa wanapoyaona. Lakini sisi tunajua kwamba mabadiliko hayo yanawezekana tu kupitia roho ya Mungu, kwa kuwa upole ni mojawapo ya matunda yenye kutokeza sana ya roho hiyo.
-
-
Onyesheni “Upole Wote Kuelekea Watu Wote”Mnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 1
-
-
2. Tunaweza kuonyeshaje “upole wote kuelekea watu wote”?
2 Upole wa kimungu ni sehemu ya matunda ya roho takatifu. Kadiri tunavyotii mwongozo wa nguvu ya utendaji ya Mungu, ndivyo tunavyodhihirisha matunda ya nguvu hiyo. Ni kwa kufanya hivyo tu tutaweza kuonyesha “upole wote” kuelekea watu wote. (Tito 3:2)
-