-
Nimebarikiwa kwa Kumtanguliza MunguAmkeni!—2009 | Machi
-
-
Mnamo 1979 tuligundua kwamba mke wangu angemzaa Jemima, kwa hiyo ikawa lazima kwetu kuacha kazi ya kuyazungukia makutaniko. Dada mdogo wa Julienne ambaye tulimwita Pépé, alikuja kutoka Benin ili aishi nasi. Familia yetu iliendelea kukua. Tulizaa wana wawili: Caleb, aliyezaliwa mnamo 1983 na Silas, aliyezaliwa mnamo 1987. Kwa hiyo, tukawa watu wanane katika familia yetu. Mimi na Julienne tulitaka kuwa wazazi wazuri, lakini pia tulitaka kubaki katika utumishi wa wakati wote ikiwa ingewezekana. Tungefanya hivyo jinsi gani? Tulikodi shamba na kupanda mihogo, mahindi, na viazi. Kisha tukajenga nyumba ndogo katika kijiji cha Ilogbo-Eremi.
Baada ya watoto kwenda shuleni, mimi na Julienne tulihubiri asubuhi. Sikuzote tulirudi nyumbani kula pamoja kama familia. Kisha, baada ya kupumzika, tulifanya kazi shambani. Pia Julienne na Pépé waliuza mazao sokoni. Sisi sote tulifanya kazi kwa bidii. Tunafurahi kwamba hatukuwa wagonjwa mara nyingi katika miaka hiyo.
-
-
Nimebarikiwa kwa Kumtanguliza MunguAmkeni!—2009 | Machi
-
-
Mnamo 1994, familia yetu ilirudi Benin, lakini Pépé, Bola, na familia zao walibaki Nigeria.
Nilifaulu kupata kazi ya muda. Kutokana na pesa tulizopata kwa kukodisha nyumba yetu huko Nigeria na msaada wenye ukarimu wa Bola, tulifaulu kujenga nyumba ambamo sisi watano tuliishi karibu na ofisi ya tawi. Jemima alitumika akiwa painia kwa zaidi ya miaka sita, akijiruzuku kwa kufanya kazi ya kushona nguo. Kisha akaolewa na Kokou Ahoumenou, na sasa wanafanya kazi katika ofisi ya tawi iliyo karibu. Hivi karibuni Caleb na Silas watamaliza shule. Kwa msaada wa Mungu na ushirikiano wa familia yetu, mimi na Julienne tumebaki katika utumishi wa wakati wote, sasa kwa zaidi ya miaka 40.
-