Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Wagalatia, Waefeso, Wafilipi, na Wakolosai
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Agosti 15
    • BAADA ya kusikia kwamba Wakristo fulani walikuwa wakipotoshwa na wafuasi wa dini ya Kiyahudi ili waiache ibada safi, mtume Paulo anaandika barua kali kwa “makutaniko ya Galatia.” (Gal. 1:2) Barua hiyo iliyoandikwa mwaka wa 50-52 W.K., ina mashauri ya moja kwa moja na himizo zito.

  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Wagalatia, Waefeso, Wafilipi, na Wakolosai
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Agosti 15
    • “KUTANGAZWA KUWA WAADILIFU”—JINSI GANI?

      (Gal. 1:1–6:18)

      Kwa kuwa wafuasi wa dini ya Kiyahudi wanajaribu kwa ujanja kumvunjia Paulo heshima, anatetea utume wake kwa kueleza habari fulani kuhusu maisha yake. (Gal. 1:11–2:14) Akipinga mafundisho yao ya uwongo, Paulo anasema hivi: “Mtu hutangazwa kuwa mwadilifu, si kwa sababu ya matendo ya sheria, bali tu kupitia imani kumwelekea Kristo Yesu.”—Gal. 2:16.

      Paulo anasema kwamba Kristo ‘aliwaachilia huru kwa kuwanunua wale walio chini ya sheria’ na kuwaweka huru ili wafurahie uhuru wa Kikristo. Anawapa Wagalatia himizo hili lenye uzito: “Simameni imara, na msijiache wenyewe kufungwa tena katika nira ya utumwa.”—Gal. 4:4, 5; 5:1.

      Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:

      3:16-18, 28, 29—Je, bado agano la Kiabrahamu ni halali? Ndiyo. Agano la Sheria halikuchukua mahali pa agano ambalo Mungu alifanya pamoja na Abrahamu, bali liliongezwa kwenye agano hilo. Hivyo, agano la Kiabrahamu liliendelea kuwapo baada ya Sheria ‘kufutwa.’ (Efe. 2:15) Ahadi zake zinapitishwa kwa “uzao” wa kweli wa Abrahamu, yaani, Kristo Yesu, ambaye ndiye sehemu ya msingi, na kwa wale “wa Kristo.”

      6:2—“Sheria ya Kristo” ni nini? Sheria hiyo inahusisha mambo yote ambayo Yesu alifundisha na kuamuru. Inatia ndani hasa amri ya ‘kupendana.’—Yoh. 13:34.

      6:8—Ni kwa njia gani ‘tunapanda kwa roho’? Tunafanya hivyo kwa kuishi kwa njia inayoiwezesha roho ya Mungu kutenda kazi kwa uhuru ndani yetu. Kupanda kwa roho kunatia ndani kushiriki kwa moyo wote katika shughuli zinazoiwezesha roho hiyo kutenda kazi kwa uhuru.

      Mambo Tunayojifunza:

      1:6-9. Matatizo yanapotokea katika kutaniko, wazee Wakristo wanapaswa kuchukua hatua ya haraka. Kwa kutoa hoja zenye kusadikisha na kutumia Maandiko, wanaweza kupinga haraka habari za uwongo.

      2:20. Fidia ni zawadi ya Mungu kwa kila mmoja wetu. Tunapaswa kuiona hivyo.—Yoh. 3:16.

      5:7-9. Mashirika mabaya yanaweza ‘kutuzuia tusiendelee kuitii kweli.’ Ni jambo la hekima kuyaepuka.

      6:1, 2, 5. Wale walio na “sifa za kustahili kiroho” wanaweza kutusaidia kubeba mzigo mzito, kama vile jambo lenye kutaabisha au tatizo zito ambalo limetokea baada ya sisi kujikwaa kwa kufanya kosa bila kujua. Lakini ni lazima sisi wenyewe tujibebee mzigo wa madaraka ya Kikristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki