-
Wale Wafalme Wawili WabadilikaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
25 Kadiri wakati ulivyopita, waliotawala baada ya Charlemagne hawakuwa na matokeo yoyote. Hata kwa muda fulani hakukuwa na maliki. Wakati huohuo, Mfalme wa Ujerumani Otto wa Kwanza alikuwa ameanza kutawala sehemu kubwa ya kaskazini na ya kati ya Italia. Akajitangaza kuwa mfalme wa Italia. Februari 2, 962 W.K., Papa John wa 12 alimtawaza Otto wa Kwanza kuwa maliki wa Milki Takatifu ya Roma. Jiji lake kuu lilikuwa Ujerumani, nao wamaliki walikuwa Wajerumani, kama vile wengi wa raia zake walivyokuwa Wajerumani. Karne tano baadaye, watawala wa Kijerumani waliotawala Austria waliitwa “maliki,” nao waliendelea kuitwa hivyo kwa muda mrefu katika ile miaka iliyosalia ya Milki Takatifu ya Roma.
WALE WAFALME WAWILI WATAMBULIKA WAZIWAZI TENA
26. (a) Ni nini kiwezacho kusemwa juu ya mwisho wa Milki Takatifu ya Roma? (b) Ni nani aliyetokea akiwa mfalme wa kaskazini?
26 Napoléon wa Kwanza aliipiga na kuiangamiza Milki Takatifu ya Roma alipokataa kutambua kuwepo kwa milki hiyo baada ya ushindi wake mbalimbali huko Ujerumani mwaka wa 1805. Kwa kuwa alishindwa kuitetea taji, Maliki Francis wa Pili alijiuzulu kutoka katika utawala wa Roma Agosti 6, 1806, na kurudia serikali yake ya kitaifa akiwa maliki wa Austria. Baada ya miaka 1,006, ile Milki Takatifu ya Roma—iliyoanzishwa na Leo wa Tatu, papa Mkatoliki, na Charlemagne, mfalme Mfaranka—ikakoma. Mwaka wa 1870, Roma likawa jiji kuu la ufame wa Italia, usiotegemea Vatikani. Mwaka uliofuata, milki ya Kijerumani ikaanza, Wilhelm wa Kwanza akateuliwa kuwa kaisari. Kwa hiyo, mfalme wa kaskazini wa kisasa—Ujerumani—akatokea duniani.
-
-
Wale Wafalme Wawili WabadilikaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 245]
1. Charlemagne 2. Napoléon wa Kwanza 3. Wilhelm wa Kwanza 4. Askari-jeshi Wajerumani, Vita ya Ulimwengu ya Kwanza
-