-
Makosa Yaliyoanzisha Vita vya UlimwenguAmkeni!—2009 | Agosti
-
-
Jambo lingine hatari lililochangia vita lilikuwa Mpango wa Schlieffen wa Ujerumani. Jina Schlieffen lilitokana na jina la aliyekuwa mkuu wa majeshi ya Ujerumani, Jenerali Alfred von Schlieffen. Mpango huo ambao ulihusisha shambulizi moja la haraka, ulitegemea wazo la kwamba Ujerumani ingelazimika kupigana na Ufaransa na Urusi. Hivyo, lengo lilikuwa kushinda Ufaransa upesi Urusi ilipokuwa ikikusanya jeshi lake polepole, kisha washambulie Urusi. “Mpango wa [Schlieffen] ulipoanzishwa, mfumo wa miungano ulihakikisha kwamba kungekuwa na vita kotekote Ulaya,” kinasema kitabu World Book Encyclopedia.
-
-
Makosa Yaliyoanzisha Vita vya UlimwenguAmkeni!—2009 | Agosti
-
-
Maliki huyo alijaribu kumhakikishia kiongozi wa Ujerumani kwamba hakutaka vita na Ujerumani. Hata hivyo, kukusanywa kwa jeshi la Urusi kulifanya Ujerumani itende kwa kasi, na Julai 31, Ujerumani ilianza kutekeleza mpango wa vita wa Schlieffen, na hivyo ikatangaza vita dhidi ya Urusi Agosti (Mwezi wa 8) 1, na siku mbili baadaye ikatangaza vita dhidi ya Ufaransa. Kwa sababu mipango ya vita ya Ujerumani ilihusisha kupitia Ubelgiji, Uingereza ilionya Ujerumani kwamba itatangaza vita dhidi yake ikiwa ingewaingiza Wabelgiji vitani. Majeshi ya Ujerumani yaliingia Ubelgiji Agosti 4. Sasa vita havingeweza kuepukwa.
-