-
Sehemu ya 3—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mambo mengi yaliyoipata familia ya Kusserow, iliyotoka Bad Lippspringe, Ujerumani, yalidhihirisha nia hiyohiyo ya kutoa ushahidi. Kielelezo kimoja chahusu jambo lililotukia baada ya Wilhelm Kusserow kuuawa hadharani katika Münster na serikali ya Nazi kwa sababu ya kukataa kwake kuridhiana imani yake. Hilda, mama yake Wilhelm, alienda gerezani mara hiyo na kusihi sana apewe mwili ili ukazikwe. Aliambia familia yake hivi: “Tutatoa ushahidi mwingi kwa watu waliomjua.” Kwenye mazishi, Franz, baba ya Wilhelm, alitoa sala iliyoonyesha imani katika uandalizi wenye upendo wa Yehova. Kaburini, Karl-Heinz, ndugu mdogo wa Wilhelm alisema maneno ya kufariji kutoka katika Biblia. Kwa kufanya hivyo waliadhibiwa, lakini kwao jambo lililokuwa la maana lilikuwa kumheshimu Yehova kwa kutoa ushahidi kuhusu jina na Ufalme wake.
-
-
Sehemu ya 3—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 449]
Familia ya Franz na Hilda Kusserow—kila mmoja wao Shahidi wa Yehova mwaminifu ingawa wote katika familia (isipokuwa mwana mmoja aliyekuwa amekufa katika aksidenti) walitiwa ndani ya kambi za mateso, magereza, au shule za kurekebishia tabia kwa sababu ya imani yao
-