-
Kujitahidi Kuwa WashindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
9. Mashahidi wa Yehova katika Ujeremani wa Nazi walitendwaje na Hitla, na kukiwa tendo-mwitikio gani kutoka viongozi wa kidini?
9 Wakati wa utawala wa Nazi katika Ujeremani, Hitla alipiga marufuku kabisa kabisa kazi ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova. Kwa miaka kadhaa, maelfu ya Mashahidi walifungwa ndani ya kambi za mateso na magereza kikatili, ambako wengi walikufa, huku wanaume vijana 200 ambao walikataa kupigana katika jeshi la Hitla wakifishwa kwa amri ya serikali. Uungaji-mkono wa viongozi wa kidini wa yote haya unathibitishwa na maneno ya padri Mkatoliki, yaliyochapishwa katika ile nyusipepa The German Way ya Mei 29, 1938. Kwa sehemu, yeye alisema: “Sasa kuna nchi moja duniani ambako wale wanaoitwa eti . . . Wanafunzi wa Biblia [Mashahidi wa Yehova] wamekatazwa. Hiyo ni Ujeremani! . . . Wakati Adolf Hitla alipochukua mamlaka, nayo Episkopati ya Kikatoliki katika Ujeremani ikarudia ombi lao, Hitla akasema: ‘Hawa wanaoitwa eti Wanafunzi wa Biblia [Mashahidi wa Yehova] Wenye Bidii ni wafanyiza matata; . . . mimi nawaona kuwa wadanganyaji; mimi sivumilii kwamba Wakatoliki Wajeremani watatupiwa matope jinsi hiyo na huyu Mwamerika Jaji Rutherford. Mimi nafumua [Mashahidi wa Yehova] katika Ujeremani.’” Kwa hayo, yule padri akaongeza: “Hongera!”
-
-
Kujitahidi Kuwa WashindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 39]
Kwa miaka mingi, wanahistoria wamekuwa wakiandaa ushahidi kuhusu ukamilifu wa Mashahidi wa Yehova Wajeremani wakati wa utawala wa Nazi. Kitabu Mothers in the Fatherland, cha mwanahistoria Claudia Koonz, kilichochapishwa 1986, kinasema: “Idadi iliyo kubwa sana ya Wajeremani wote kutoka asili zisizo za Kinazi walipata njia za kuishi chini ya utawala waliodharau. . . . Kwenye ule upande mwingine wa spektra ya kitakwimu na ya kiitikadi walikuwako Mashahidi wa Yehova 20,000, ambao, karibu kila mmoja wao, walikataa katakata kutoa namna yoyote ya utii kwa serikali ya Nazi. . . . Kikundi chenye kushikamana zaidi ya vyote cha wakinzani kilitegemezwa na dini. Tangu mwanzo, Mashahidi wa Yehova hawakushirikiana na sehemu yoyote ya serikali ya Nazi. Hata baada ya Gestapo kuharibu makao makuu yao ya taifa katika 1933 na wakapiga marufuku farakano hilo katika 1935, wao walikataa kufanya jambo hata lililo dogo kama vile kusema ‘Heil Hitler.’ Wapatao nusu (zaidi wakiwa wanaume) wa Mashahidi wa Yehova wote walipelekwa kwenye kambi za mateso, elfu moja yao walifishwa, na elfu nyingine ikafa kati ya 1933 na 1945. . . . Wakatoliki na Waprotestanti walisikia viongozi wao wa kidini wakiwahimiza washirikiane na Hitla. Ikiwa wao walipinga, wao walifanya hivyo kinyume cha maagizo kutoka kwa kanisa na serikali pia.”
-