-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ghana
Kukiwa na ongezeko kubwa la simu za mkononi sehemu nyingi za Afrika, inasemekana kwamba tunaishi katika “enzi ya mawasiliano.” Ili kuwahamasisha wateja wa simu, kampuni nyingi za simu huwapa wateja muda wa kupiga simu bila malipo wakati fulani wa usiku. Dada mmoja anayeitwa Grace, aliamua kutumia vizuri huduma hiyo. Haikuwa rahisi kwake kujifunza na Monica, kwa sababu sikuzote Monica alikuwa na shughuli nyingi. Grace alifanya yote awezayo ili aendelee kujifunza na Monica, hata akapanga kumtembelea saa 11 alfajiri. Hata hivyo, ratiba ya Monica ilibadilika, ikawa vigumu kujifunza wakati huo. Grace aliamua kutumia huduma ya kupiga simu usiku bila malipo. Monica alikubali, nao wakapanga kujifunza saa 10 usiku kupitia simu. Walivunjika moyo walipogundua kwamba wakati huo watu wengi sana wanautumia mtandao na si rahisi kupiga simu. Kwa hiyo, wakapanga kuamka mapema hata zaidi ili wajifunze saa 9 usiku, ingawa haikuwa rahisi kufanya hivyo kwa kuwa wote wawili ni wafanyakazi. Grace anasema: “Nilimwomba Yehova anipe nguvu na uwezo wa kuendelea ili upendezi wa mwanafunzi wangu usipoe. Nilitega kengele ya simu yangu ili niamke na kuazimia kuwa macho wakati huo. Ijapokuwa nilikuwa na uchovu mwingi, nilijipa moyo.” Jitihada zake zilimletea shangwe kubwa alipomwona Monica akibatizwa katika Kusanyiko la Wilaya la “Kuongozwa na Roho ya Mungu” la mwaka wa 2008! Hivi karibuni, Grace ametumia huduma hiyohiyo ya kupiga simu usiku bila malipo kujifunza na mwanamke fulani ambaye sasa ameanza kuhudhuria mikutano.
-
-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 45]
Dada alijidhabihu na kutumia tekinolojia ya kisasa ili kuongoza funzo la Biblia
-