-
Maisha Yenye Kuthawabisha Katika Utumishi wa YehovaMnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 1
-
-
Kabla tu ya kuanzishwa kwa shule ya Gileadi, mimi pamoja na wengine wawili kutoka Betheli tulipewa mgawo wa kutembelea makutaniko kotekote Marekani. Tuliyatembelea makutaniko kwa siku moja, siku kadhaa au hata juma zima katika juhudi za kuyaimarisha kiroho. Tuliitwa watumishi wa akina ndugu, jina ambalo baadaye lilibadilishwa kuwa watumishi wa mzunguko, au waangalizi wa mzunguko. Baada tu ya kuanzishwa kwa Shule ya Gileadi, niliombwa nirudi ili nifundishe masomo kadhaa. Nilifunza darasa la 2 hadi la 5, na pia nikawa mwalimu-badala katika darasa la 14. Kuzungumzia pamoja na wanafunzi matukio ya mapema katika historia ya kisasa ya tengenezo la Yehova—mengi yakiwa matukio niliyojionea—yalinifanya nithamini sana urithi wangu wa kiroho wenye kuthawabisha.
-
-
Maisha Yenye Kuthawabisha Katika Utumishi wa YehovaMnara wa Mlinzi—2001 | Novemba 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 23]
Nikifundisha darasa la Gileadi mwaka wa 1945
Juu kulia: Walimu wa Shule ya Gileadi Eduardo Keller, Fred Franz, mimi, na Albert Schroeder
-