Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Pokea kwa Shukrani Toa kwa Moyo Wote
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
    • Changia Hali Njema ya Kutaniko

      Bila shaka, utakubali kwamba umefaidika katika njia nyingi kwa sababu ya kushirikiana na kutaniko la Kikristo. Yehova ameandaa chakula kingi cha kiroho kupitia kutaniko. Ulipata kweli ambayo ilikuweka huru kutokana na uwongo wa kidini na giza la kiroho. (Yoh. 8:32) Katika mikutano ya Kikristo na makusanyiko yaliyotayarishwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ulipata ujuzi ambao utakusaidia kupata uzima wa milele katika dunia paradiso ambayo haitakuwa na uchungu wala maumivu. (Mt. 24:45-47) Je, kweli unaweza kuhesabu faida zote ambazo umepata, na zile ambazo utapata kupitia kutaniko la Mungu? Unaweza kulishukuru kutaniko jinsi gani?

      Mtume Paulo aliandika hivi: “Mwili wote, kwa kuunganishwa pamoja kwa upatano na kufanywa ushirikiane kupitia kila kiungo ambacho hutoa kile kinachohitajiwa, kulingana na utendaji wa kila kiungo kimoja-kimoja katika kipimo kinachofaa, hutokeza ukuzi wa mwili ili huo ujijenge wenyewe katika upendo.” (Efe. 4:15, 16) Ingawa andiko hilo linahusu hasa jamii ya Wakristo watiwa-mafuta, kanuni hiyo inaweza kutumiwa na Wakristo wote leo. Ndiyo, kila mshiriki wa kutaniko anaweza kuchangia hali njema na ukuzi wa kutaniko. Tunaweza kufanya hivyo katika njia gani?

      Tunaweza kufanya hivyo kwa kujitahidi kabisa nyakati zote kuwatia moyo na kuwaburudisha wengine kiroho. (Rom. 14:19) Pia, tunaweza kuchangia katika “ukuzi wa mwili” kwa kusitawisha matunda ya roho ya Mungu katika shughuli zetu zote pamoja na waamini wenzetu. (Gal. 5:22, 23) Kwa kuongezea, tunaweza kutafuta nafasi za ‘kuwatendea wote mema, na hasa wale ambao katika imani ni jamaa zetu.’ (Gal. 6:10; Ebr. 13:16) Kila mtu kutanikoni, yaani, ndugu na dada, wachanga na wale ambao ni wazee kwa umri, wanaweza kushiriki katika ‘kuujenga mwili katika upendo.’

      Zaidi ya hayo, tunaweza kutumia vipawa, nguvu na mali zetu katika kazi ya kuokoa uhai inayofanywa na kutaniko. Yesu Kristo alisema, “Mlipokea bure.” Nasi tunapaswa kutenda jinsi gani? “Toeni bure,” akasema. (Mt. 10:8) Kwa hiyo, shiriki kikamili katika kazi ya maana sana ya kuhubiri kuhusu Ufalme na kufanya wanafunzi. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Je, kuna hali fulani zinazokuzuia usitimize mengi? Mkumbuke yule mjane mwenye uhitaji aliyetajwa na Yesu. Alitoa mchango mdogo sana. Hata hivyo, Yesu alisema kwamba alitoa zaidi ya wengine wote. Alitoa yote kulingana na hali zake.—2 Kor. 8:1-5, 12.

  • Pokea kwa Shukrani Toa kwa Moyo Wote
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 31]

      “Nitamlipa Yehova nini kwa ajili ya faida zake zote kwangu?”—Zab. 116:12

      ▪ Tafuta nafasi za ‘kuwatendea wote mema’

      ▪ Watie moyo na kuwaburudisha wengine kiroho

      ▪ Shiriki kikamili katika kazi ya kufanya wanafunzi kadiri hali zako zinavyokuruhusu

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki