-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kwenye Mataifa Yenye Nderemo Kusanyiko la Kitheokrasi, lililofanywa katika Cleveland, Ohio, Agosti 4-11, 1946, Ndugu Knorr alitoa hotuba yenye kichwa “Wenye Kupatiwa Vifaa kwa Ajili ya Kila Kazi Njema.” Hamu ya wasikilizaji wote iliamshwa alipouliza maswali kama vile: “Je, haungekuwa usaidizi mkubwa kupata habari juu ya kila kimojapo vitabu sitini na sita vya Biblia? Je, isingesaidia kuelewa Maandiko kama tungejua ni nani aliyeandika kila kitabu cha Biblia? ni wakati gani kila kitabu kiliandikwa? ni wapi kilikoandikiwa?” Tarajio likapanda alipojulisha: “Akina ndugu, mna habari hiyo yote na zaidi katika kitabu hiki kipya chenye kichwa ‘Equipped for Every Good Work’!” Makofi ya ghafula yakafuata tangazo hilo. Kichapo hicho kipya kingetumika kikiwa kitabu cha mafundisho kwa ajili ya shule ya huduma iliyofanywa katika makutaniko.
Mashahidi wa Yehova hawakupewa tu kichapo hicho ili kuupa kina ujuzi wao wa Maandiko bali pia walipewa misaada bora ya kutumia shambani. Mkusanyiko wa 1946 utakumbukwa kwa muda mrefu kwa kutolewa kwa toleo la kwanza la Amkeni! Gazeti hilo jipya lilichukua mahali pa Consolation (lililoitwa hapo kwanza The Golden Age). Pia kitabu “Let God Be True”e kilitolewa. Henry A. Cantwell, ambaye baadaye alitumikia akiwa mwangalizi asafiriye, aeleza hivi: “Kwa wakati fulani tulikuwa tumehitaji sana kitabu ambacho kingeweza kutumiwa kwa mafanikio katika kuongoza mafunzo ya Biblia pamoja na watu wapya wenye kupendezwa, ambacho kingezungumzia mafundisho na kweli za msingi za Biblia. Sasa kwa kutolewa ‘Let God Be True,’ tulikuwa na kitu kile hasa tulichohitaji.”
Wakiwa na misaada ya kufundishia yenye thamani hivyo, Mashahidi wa Yehova walitarajia mpanuko zaidi wa haraka sana. Akihutubia mkusanyiko juu ya kichwa “Matatizo ya Kujenga Upya na Upanuzi,” Ndugu Knorr alieleza kwamba wakati wa miaka ya vita ya duniani pote, jitihada za kutoa ushahidi hazikusimama. Kutoka 1939 kufika 1946, idadi ya wapiga-mbiu wa Ufalme ilikuwa imeongezeka kwa zaidi ya 110,000. Ili kutimiza mahitaji yenye kuongezeka ya fasihi ya Biblia, Sosaiti ilikuwa inapanga kupanua kiwanda na Kao la Betheli katika Brooklyn.
Kipindi kilichotarajiwa cha amani ya ulimwengu kilikuwa kimeanza. Ile enzi ya mpanuko wa duniani pote na elimu ya Biblia ilikuwa imeanza kuwa na maendeleo mazuri. Mashahidi wa Yehova walirudi nyumbani kutoka Mataifa Yenye Nderemo Kusanyiko la Kitheokrasi wakiwa wamepatiwa vifaa vizuri zaidi ili wawe walimu wa habari njema.
-
-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Vikiwa vimejengwa kwa utegemezo wa kifedha wa Mashahidi kutoka kote ulimwenguni, vifaa hivyo vipya vilikamilisha ule mradi wa mpanuko mkubwa mno uliotangazwa na kukubaliwa kwa idili kwenye mkusanyiko wa Cleveland wa 1946.
-