-
Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu WetuMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mwaka uliofuata, 1946, akina ndugu katika Ujerumani walipanga kuwe na mkusanyiko katika Nuremberg. Waliruhusiwa kutumia Zeppelinwiese, zilizokuwa hapo kwanza nyanja za kufanyia gwaride za Hitler. Katika siku ya pili ya mkusanyiko, Erich Frost, ambaye alikuwa amepatwa kibinafsi na unyama wa Gestapo na alikuwa ametumia miaka kadhaa katika kambi ya mateso ya Nazi, alitoa hotuba ya watu wote “Wakristo Watahiniwa Vikali.” Watu 3,000 kati ya umma wa Nuremberg walijiunga na wale Mashahidi 6,000 waliohudhuria kwa pindi hiyo.
Siku ya mwisho ya mkusanyiko ilithibitika kuwa wakati ambapo hukumu zingetangazwa kwenye majaribio ya uhalifu wa wakati wa vita huko katika Nuremberg. Wenye mamlaka wa kijeshi walitangaza kafyu kwa siku hiyo, lakini baada ya mazungumzo marefu walikubali kwamba kwa sababu ya msimamo ambao Mashahidi wa Yehova walichukua ujapokuwa upinzani wa Nazi, haingefaa kuwazuia wasimalizie mkusanyiko wao kwa amani. Hivyo, katika siku hiyo ya mwisho, ndugu walikusanyika wasikie ile hotuba yenye kuchochea hisia “Wasio na Hofu Ijapokuwa Njama ya Ulimwengu.”
Waliona mkono wa Yehova katika yale yaliyokuwa yakitukia. Wakati uleule ambao wanaume waliowakilisha utawala wa kimabavu uliokuwa umejaribu kuwaangamiza walipokuwa wakihukumiwa, Mashahidi wa Yehova walikuwa wakikutana kumwabudu Yehova mahali penyewe ambapo Hitler alikuwa ameonyesha nguvu zake za Kinazi zenye kutazamisha. Mwenyekiti wa mkusanyiko alisema: “Kuweza kuona tu siku hii, ambayo ni ono tu la kimbele la ushindi wa watu wa Mungu juu ya maadui wao kwenye vita ya Har–Magedoni, ilistahilisha miaka tisa ya kuwa katika kambi ya mateso.”
-
-
Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu WetuMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 268]
Katika Nuremberg, Ujerumani, mwaka 1946, Erich Frost alitoa hotuba motomoto “Wakristo Watahiniwa Vikali”
-