Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Wewe Hutamani Kutumikia Kikamili Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Machi 15
    • Weka Miradi Iwezayo Kufikiwa

      Kuridhika kwetu na mapendeleo ya sasa ya utumishi hakumaanishi kwamba tukome kuweka miradi zaidi ya kitheokrasi. Akizungumza juu ya ufufuo wa kimbingu, Paulo alisema juu ya “kujinyoosha mbele kwenye mambo ya mbele.” Pia alisema hivi: “Kwa kadiri ambayo tumefanya maendeleo, acheni tuendelee kutembea kwa utaratibu katika kawaida hiyohiyo.” (Wafilipi 3:13-16) Miradi ya kitheokrasi yaweza kutusaidia kujinyoosha mbele. Hata hivyo, jambo lililo gumu ni kudumisha miradi hiyo ikiwa halisi.

      Miradi halisi ni yenye kufaa na iwezayo kufikiwa. (Wafilipi 4:5) Hilo halimaanishi kwamba mradi unaohitaji miaka mingi ya kazi ngumu si halisi. Mradi huo wa muda mrefu waweza kufikiwa hatua kwa hatua kwa kuweka mfululizo wa miradi ya katikati, au hatua. Hatua hizo zaweza kutumika zikiwa vitia alama maendeleo ya kiroho. Kumaliza kila hatua kwa mafanikio kutaandaa kwa wakati uliopo hali ya uradhi badala ya mtamauko.

      Usawaziko Mzuri

      Hata hivyo, ni jambo la maana kutambua kwamba kwa sababu ya hali zetu na mipaka yetu, mapendeleo fulani huenda yasipokewe. Kuyaweka kuwa miradi huongoza tu kwenye mtamauko na kuvunjika moyo. Miradi kama hiyo yapasa kuahirishwa, angalau kwa wakati uliopo. Haitakuwa vigumu kufanya hivyo, tukisali kupata uradhi wa kimungu na kufanya hangaiko letu kuu kuwa kufanya mapenzi ya Yehova. Tujaribupo kufikia mapendeleo, utukufu wa Yehova—wala si kutambuliwa kwa matimizo yetu ya kibinafsi—ndilo jambo la maana. (Zaburi 16:5, 6; Mathayo 6:33) Kwa kufaa Biblia hutuambia hivi: “Mkabidhi BWANA kazi zako, na mawazo yako yatathibitika.”—Mithali 16:3.

  • Je, Wewe Hutamani Kutumikia Kikamili Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Machi 15
    • Miradi Tuwezayo Kuweka

      Kusoma Biblia kila siku.—Yoshua 1:8; Mathayo 4:4

      Kuboresha nguvu zetu za ufahamu kupitia kujizoeza Kimaandiko.—Waebrania 5:14

      Kukuza uhusiano wa karibu zaidi pamoja na Mungu.—Zaburi 73:28

      Kusitawisha kila moja la matunda ya roho.—Wagalatia 5:22, 23

      Kuboresha sala zetu.—Wafilipi 4:6, 7

      Kuwa wenye matokeo zaidi katika kuhubiri na kufundisha.—1 Timotheo 4:15, 16

      Kusoma na kutafakari kila toleo la magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Zaburi 49:3

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki