-
Njia za Kupanua Huduma YakoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
mzuri ambaye hali zake zinamruhusu kutumia saa hususa kuhubiri habari njema. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko huidhinisha maombi ya utumishi wa upainia msaidizi na wa kawaida, nayo ofisi ya tawi huweka rasmi mapainia wa pekee.
12 Mhubiri anaweza kuwa painia msaidizi kwa angalau mwezi mmoja, miezi kadhaa mfululizo, au kwa kuendelea, ikitegemea hali zake. Wahubiri wengi wa Ufalme hufanya upainia msaidizi katika pindi za pekee, kama vile majira ya Ukumbusho au mwezi wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Wengine huamua kuwa mapainia wakati wa likizo. Wahubiri waliobatizwa wanaosoma wanaweza kujiandikisha kuwa mapainia wasaidizi shule zinapofungwa. Wahubiri wanaweza kuchagua kuwa mapainia wasaidizi kwa punguzo la takwa la saa kila mwezi wa Machi na Aprili na mwezi wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Hata hali zako ziweje, ikiwa una maadili mazuri, ikiwa unaweza kupanga kutimiza takwa lililowekwa la saa, na unaamini kwamba unaweza kutumikia kwa mwezi mmoja au zaidi ukiwa painia msaidizi, wazee watafurahia kufikiria ombi lako la kushiriki katika pendeleo hilo la utumishi.
13 Ili ustahili kuwa painia wa kawaida, unapaswa kuwa na uwezo wa kutimiza takwa la saa kwa mwaka. Ukiwa painia wa kawaida, unapaswa kushirikiana kwa ukaribu na kutaniko lenu. Mapainia wenye bidii ni baraka kutanikoni, huwachochea wahubiri washiriki katika huduma ya shambani na hata kuwatia moyo wawe mapainia. Hata hivyo, kabla ya kujaza ombi la kuwa painia wa kawaida, lazima uwe umebatizwa angalau miezi sita iliyopita na uwe mhubiri mwenye mfano mzuri.
14 Kwa kawaida mapainia wa pekee huchaguliwa kati ya mapainia wa kawaida ambao wamekuwa na matokeo mazuri katika huduma. Lazima wawe na hali zitakazowaruhusu kutumikia popote ambapo ofisi ya tawi itawatuma. Mara nyingi wao hutumwa kwenye maeneo ya mbali ili watafute watu wanaopendezwa na kuanzisha makutaniko mapya. Nyakati nyingine, mapainia wa pekee hutumwa kwenye makutaniko yanayohitaji kusaidiwa kuhubiri eneo lao kubwa. Baadhi ya mapainia wa pekee ambao pia ni wazee hutumwa ili kusaidia makutaniko madogo, hata yasiyo na uhitaji hususa wa kuhubiri. Mapainia wa pekee hupokea pesa kidogo ili kugharimia mahitaji yao. Baadhi ya mapainia wa pekee huwekwa rasmi kwa muda.
WAMISHONARI
15 Halmashauri ya Utumishi ya Baraza Linaloongoza huwaweka rasmi wamishonari, kisha Halmashauri ya Tawi ya nchi wanayotumikia huwapa mgawo wa kuhubiri katika maeneo yenye watu wengi. Wao hutimiza mengi katika kuimarisha kazi ya kuhubiri na kuyatia nguvu makutaniko. Kwa kawaida, wamishonari huzoezwa kwenye Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Wao hupewa makao na pesa kidogo ili kugharimia mahitaji yao.
KAZI YA MZUNGUKO
16 Wale wanaowekwa rasmi na Baraza Linaloongoza kuwa waangalizi wa mzunguko hupata mazoezi na uzoefu kwanza kwa kutumikia wakiwa waangalizi badala wa mzunguko. Wanaume hao wanaipenda huduma na ndugu zao pia. Ni mapainia wenye bidii, wanajifunza Biblia kwa bidii, na ni wasemaji na walimu wazuri. Wanaonyesha kwa kiwango kikubwa tunda la roho, ni wenye usawaziko na busara. Ikiwa ndugu ameoa, mkewe anapaswa kuwa painia mwenye mwenendo mzuri anayewatendea wengine vizuri. Ni mhubiri mwenye matokeo mazuri. Pia, anatambua wajibu wake wa kujitiisha akiwa mke Mkristo, hazungumzi kwa niaba ya mumewe au kutawala mazungumzo. Waangalizi wa mzunguko na wake zao huwa na ratiba yenye mambo mengi, kwa hiyo wale wanaojitahidi kufikia utumishi huo wanapaswa kuwa na afya nzuri. Mapainia hawatumi maombi ya kufanya kazi ya mzunguko. Badala yake, wanamwambia mwangalizi wao wa mzunguko tamaa yao, naye huwapa madokezo ya kufikia pendeleo hilo.
SHULE ZA KITHEOKRASI
17 Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme: Waeneza-injili zaidi wa Ufalme wanahitajiwa ili kuhubiri maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida na kuimarisha makutaniko kiroho. Kwa hiyo, ndugu na dada waseja na wenzi wa ndoa wanaweza kujaza maombi ya kupata mazoezi ya pekee katika Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Baada ya kuhudhuria shule hiyo, wahitimu hutumwa wakiwa mapainia wa kawaida kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa katika nchi yao. Hata hivyo, wale ambao hali zao zinawaruhusu wanaweza kupewa migawo mingine nchini mwao au katika nchi nyingine. Huenda wachache wakatumwa wakiwa mapainia wa pekee wa muda au wa kudumu. Mapainia ambao wangependa kuhudhuria shule hii wanaweza kujua matakwa kwenye mkutano unaofanywa wakati wa kusanyiko la eneo.
18 Shule ya Gileadi: Ndugu na dada waseja na wenzi wa ndoa wanaochaguliwa kuhudhuria shule hii wanazungumza Kiingereza na wanatumikia wakiwa watumishi wa pekee wa wakati wote. Wana uwezo wa kuimarisha kazi ya kuhubiri au kutumikia kwenye ofisi ya tawi. Tayari wameonyesha kwamba wanafurahia kuwatumikia ndugu zao na wanaweza kuwasaidia wengine kwa fadhili kujifunza na kufuata mwongozo wa Kimaandiko na wa kitheokrasi. Halmashauri ya Tawi huwaomba wanafunzi watume maombi. Wahitimu wa shule hii hupewa mgawo wa kuhubiri au kutumikia kwenye ofisi ya tawi katika nchi yao au nchi nyingine.
UTUMISHI WA BETHELI
19 Kutumikia Betheli ni pendeleo la pekee. Jina Betheli linamaanisha “Nyumba ya Mungu,” na vituo hivyo vya utendaji wa kitheokrasi vinastahili kabisa kuitwa hivyo. Ndugu na dada wanaotumikia Betheli hufanya kazi muhimu inayohusisha kutayarisha, kutafsiri, na kusambaza machapisho ya Biblia. Utumishi wao unathaminiwa sana na Baraza Linaloongoza, ambalo husimamia na kuelekeza makutaniko duniani kote. Wanabetheli wengi ambao ni watafsiri, huishi na kufanya kazi katika maeneo ya ofisi yao ya tawi ambayo lugha wanayotafsiri huzungumzwa. Hilo huwasaidia kusikia lugha hiyo ikizungumzwa katika shughuli za kila siku. Pia, wanaweza kujionea ikiwa watu wanaelewa lugha iliyotumiwa katika machapisho yaliyotafsiriwa.
20 Kazi nyingi inayofanywa Betheli inahitaji nguvu nyingi. Kwa hiyo, hasa ndugu vijana waliojiweka wakfu na kubatizwa, wenye nguvu na afya nzuri ndio wanaoitwa Betheli. Ikiwa kuna uhitaji katika ofisi ya tawi inayosimamia nchi yenu na ungependa kutumikia Betheli, unaweza kupata habari zaidi kuhusu matakwa unayopaswa kutimiza kutoka kwa wazee wa kutaniko lako.
KUTUMIKIA KATIKA KAZI YA UJENZI
21 Ujenzi wa majengo ya kitheokrasi ni utumishi mtakatifu, kama ule uliofanywa wakati wa ujenzi wa hekalu la Sulemani. (1 Fal. 8:13-18) Ndugu na dada wengi huonyesha bidii ya pekee kwa kutumia wakati na mali zao ili kushiriki katika kazi hiyo.
22 Je, unaweza kusaidia? Ikiwa wewe ni mhubiri aliyebatizwa na ungependa kushiriki katika kazi hiyo, ndugu wanaosimamia ujenzi katika eneo lenu watathamini msaada wako, na ikiwa huna ujuzi watakuzoeza. Ikiwa ungependa kusaidia, kwa nini usiwajulishe wazee? Baadhi ya wahubiri wanaostahili wamejitolea kushiriki katika ujenzi wa majengo ya kitheokrasi katika nchi nyingine.
23 Kuna fursa nyingi za kushiriki katika utumishi wa ujenzi. Wahubiri waliobatizwa ambao ni mfano mzuri na wana ujuzi fulani, wanaweza kujitolea katika maeneo yaliyo karibu na kwao wakitumikia wakiwa wajitoleaji wa Idara ya Usanifu-Majengo na Ujenzi. Wengine wanaweza kwenda kujitolea maeneo ya mbali na kwao kwa kipindi fulani cha wakati, na hutumwa na ofisi ya tawi kwa majuma mawili hadi miezi mitatu wakitumikia wakiwa wajitoleaji wa ujenzi. Wale wanaotumwa na ofisi ya tawi kutumikia kwa muda mrefu wanaitwa watumishi wa ujenzi. Mtumishi wa ujenzi anayepewa mgawo katika nchi nyingine anaitwa mtumishi wa ujenzi kutoka nchi nyingine. Kikundi cha Ujenzi kinafanyizwa na watumishi na wajitoleaji wa ujenzi na huongoza katika kila mradi wa ujenzi kikisaidiwa na wajitoleaji wa Idara ya Usanifu-Majengo na Ujenzi wa eneo hilo pamoja na wajitoleaji kutoka kutaniko ambalo ujenzi unafanywa. Vikundi vya Ujenzi huhama kutoka mradi mmoja hadi mwingine ulio chini ya usimamizi wa ofisi ya tawi.
UNA MALENGO GANI YA KIROHO?
24 Ikiwa umejiweka wakfu kwa Yehova, bila shaka unatamani kumtumikia milele. Hata hivyo, kwa sasa una malengo gani ya kiroho? Kuwa na malengo ya kiroho kutakusaidia utumie nguvu na mali zako kwa hekima. (1 Kor. 9:26) Kujiwekea malengo kama hayo hukusaidia kukua kiroho na kutakusaidia kuzingatia mambo muhimu zaidi unapojitahidi kufikia mapendeleo mengine ya utumishi.—Flp. 1:10; 1 Tim. 4:15, 16.
25 Mtume Paulo alituwekea mfano mzuri wa kuiga tunapomtumikia Mungu. (1 Kor. 11:1) Paulo alijitahidi sana kumtumikia Yehova. Alitambua kwamba Yehova alikuwa amempa nafasi nyingi za kumtumikia. Paulo aliwaandikia hivi ndugu huko Korintho: “Nimefunguliwa mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji.” Je, sivyo ilivyo kwetu pia? Naam, tuna nafasi nyingi za kumtumikia Yehova tunaposhirikiana na kutaniko, hasa katika kuhubiri habari njema ya Ufalme. Lakini kama Paulo, tunatambua kwamba kupita katika ‘mlango huo mkubwa’ kunahusisha kukabiliana na “wapinzani wengi.” (1 Kor. 16:9) Paulo alikuwa tayari kujitia nidhamu. Ona alivyosema: “Naupigapiga mwili wangu na kuuongoza kama mtumwa.” (1 Kor. 9:24-27) Je, unamwiga Paulo?
Kuwa na malengo ya kiroho kutakusaidia utumie nguvu na mali zako kwa hekima
26 Kila mmoja wetu anaweza kujiwekea malengo ya kitheokrasi kulingana na hali zake. Wengi wanashiriki katika utumishi wa wakati wote kwa sababu walijiwekea malengo ya kitheokrasi mapema maishani. Walipokuwa bado watoto, wazazi wao waliwatia moyo wajiwekee malengo. Hivyo, wamefurahia baraka nyingi katika utumishi wa Yehova na hawajuti kamwe. (Met. 10:22) Malengo mengine mazuri tunayoweza kujiwekea ni kama vile kushiriki katika utumishi wa shambani kila juma, kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia, au kutenga wakati zaidi wa kutayarisha mikutano. Jambo muhimu ni kubaki washikamanifu na kutimiza huduma yetu kikamili. Tukifanya hivyo, tutamletea Yehova sifa na kufikia lengo letu kuu zaidi la kumtumikia milele.—Luka 13:24; 1 Tim. 4:7b, 8.
-
-
Mipango ya Mahali pa IbadaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 11
Mipango ya Mahali pa Ibada
WAABUDU wa kweli wa Yehova wanaamuriwa wakusanyike pamoja ili wafundishwe na watiane moyo. (Ebr. 10:23-25) Mahali pa kwanza ambapo Waisraeli, watu waliochaguliwa na Mungu, walikusanyika kwa ajili ya ibada paliitwa “hema la ibada, yaani, hema la mkutano.” (Kut. 39:32, 40) Baadaye, Sulemani mwana wa Daudi alijenga nyumba, au hekalu, kwa utukufu wa Mungu. (1 Fal. 9:3) Baada ya hekalu hilo kuharibiwa mwaka wa 607 K.W.K., Wayahudi walipanga kukutana kwenye majengo yaliyoitwa masinagogi ili kumwabudu Mungu. Baada ya muda, hekalu lilijengwa tena, na kwa mara nyingine likawa kituo cha ibada ya kweli. Yesu alifundisha kwenye masinagogi na pia hekaluni. (Luka 4:16; Yoh. 18:20) Yesu alifanya mkutano hata kwenye mlima.—Mt. 5:1–7:29.
2 Baada ya Yesu kuuawa, Wakristo walikusanyika katika sehemu za umma na kwenye nyumba za watu ili kufundisha Maandiko na kushirikiana na waamini wenzao. (Mdo. 19:8, 9; Rom. 16:3, 5; Kol. 4:15; Flm. 2) Nyakati nyingine Wakristo wa karne ya kwanza walilazimika kukutana mahali ambapo hapakuwa na watu ili kuwaepuka watesaji. Kwa kweli, zamani watumishi waaminifu wa Mungu walitamani sana kukusanyika mahali pa ibada ili ‘kufundishwa na Yehova.’—Isa. 54:13.
3 Leo pia, sehemu za umma na nyumba za watu hutumiwa kwa ajili ya mikutano ya Kikristo. Mara nyingi nyumba za watu hutumiwa kwa ajili ya mikutano ya utumishi wa shambani. Wale wanaoruhusu mikutano hiyo ifanywe kwenye nyumba zao huliona hilo kuwa pendeleo kubwa. Wengi wanaona kwamba wamenufaika kiroho kwa kuruhusu nyumba zao zitumiwe.
JUMBA LA UFALME
4 Mashahidi wa Yehova hukutana hasa kwenye Jumba la Ufalme. Kwa kawaida, uwanja hununuliwa kisha Jumba jipya la Ufalme hujengwa, au jengo fulani linanunuliwa na kufanyiwa marekebisho. Inapowezekana, makutaniko kadhaa yanaweza kutumia Jumba moja la Ufalme ili kupunguza gharama na kulitumia kwa ukamili. Katika maeneo mengine, inalazimu kukodi jumba. Jumba jipya la Ufalme likijengwa au kufanyiwa ukarabati mkubwa, inafaa liwekwe wakfu. Hata hivyo, ikiwa Jumba la Ufalme limefanyiwa marekebisho au ukarabati mdogo tu, basi hakuna haja ya kuliweka wakfu.
5 Jumba la Ufalme halipaswi kuwa jengo lenye madoido ili kuwavutia watu. Ingawa huenda muundo wake ukatofautiana ikitegemea eneo, sikuzote majengo hayo hutimiza kusudi linalofaa. (Mdo. 17:24) Ikitegemea hali, jumba linapaswa kuwa zuri na mahali panapofaa kufanyiwa mikutano ya Kikristo.
6 Makutaniko yote ya Mashahidi wa Yehova huchangia gharama za matumizi, uendeshaji, na udumishaji wa Jumba lao la Ufalme. Hakuna sadaka zinazokusanywa; wala Mashahidi hawachangishi pesa kutoka kwa watu. Kuna sanduku la michango kwa ajili ya wahudhuriaji ambao huenda wangependa kuchangia gharama muhimu za matumizi ya jumba hilo. Wanachangia kwa hiari na kutoka moyoni.—2 Kor. 9:7.
7 Washiriki wote wa kutaniko hufurahia kuchangia pesa na kujitolea kulisafisha na kulidumisha Jumba la Ufalme. Kwa kawaida mzee au mtumishi wa huduma hupewa mgawo wa kuratibu kazi hiyo. Mara nyingi usafi hufanywa na vikundi vya utumishi, chini ya uongozi wa mwangalizi wa kikundi au msaidizi wake. Iwe ni ndani au nje, Jumba la Ufalme linapaswa kumwakilisha Yehova na tengenezo lake kwa njia inayofaa.
Washiriki wote wa kutaniko hufurahia kuchangia pesa na kujitolea kulisafisha na kulidumisha Jumba la Ufalme
8 Mahali ambako makutaniko kadhaa yanatumia jumba moja, wazee wa makutaniko yanayohusika huunda Halmashauri ya Uendeshaji wa Jumba la Ufalme, ili kusimamia mambo yote yanayohusiana na jengo na uwanja wa jumba. Mabaraza ya wazee humteua ndugu mmoja kuwa mratibu wa halmashauri ya uendeshaji. Ikifanya kazi chini ya mwelekezo wa mabaraza ya wazee, halmashauri hiyo husimamia usafi wa jumba, na kuhakikisha kwamba linatunzwa vizuri na kuna vifaa vya kutosha. Ili kufanikisha hilo makutaniko yanayohusika yanapaswa kushirikiana.
9 Makutaniko kadhaa yanapotumia Jumba moja la Ufalme, huenda ratiba ya mikutano ikabadilika-badilika. Wazee wanapopanga ratiba hiyo wanapaswa kuchochewa na roho ya ufikirio na upendo. (Flp. 2:2-4; 1 Pet. 3:8) Kutaniko moja halipaswi kufanya uamuzi kwa niaba ya makutaniko mengine. Mwangalizi wa mzunguko anapotembelea mojawapo ya makutaniko hayo, makutaniko mengine katika jumba hilo yatabadili muda wa mikutano yao katika juma hilo.
10 Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ikiidhinisha, Jumba la Ufalme linaweza kutumiwa kwa ajili ya hotuba ya ndoa na ya maziko. Wazee hao hufikiria ombi lililotolewa kwa uangalifu na kufanya uamuzi kupatana na mwongozo wa ofisi ya tawi.
11 Wale wanaoruhusiwa kutumia Jumba la Ufalme kwa makusudi hayo wanapaswa kujiendesha kwa njia ya Kikristo. Hakuna jambo linalopaswa kufanyika katika Jumba la Ufalme ambalo litaudhi kutaniko au kumletea Yehova suto na kuharibu sifa nzuri ya kutaniko. (Flp. 2:14, 15) Chini ya mwelekezo wa ofisi ya tawi, Jumba la Ufalme linaweza kutumiwa kwa shughuli nyingine za kiroho, kama vile Shule ya Huduma ya Ufalme na Shule ya Utumishi wa Painia.
12 Nyakati zote kutaniko linapaswa kuheshimu mahali pa mikutano. Mavazi, mapambo na tabia zinapaswa kuonyesha heshima inayostahili ibada ya Yehova. (Mhu. 5:1; 1 Tim. 2:9, 10) Tunaonyesha kwamba tunathamini mikutano yetu ya Kikristo tunapotii ushauri huo.
13 Ni muhimu kudumisha utaratibu mikutano inapoendelea. Inapendekezwa kwamba watoto waketi pamoja na wazazi wao. Wazazi wenye watoto wadogo wanatiwa moyo kuketi mahali ambapo hawatawakengeusha sana wasikilizaji ikiwa watahitaji kuwatoa nje watoto wao ili kuwatia nidhamu au kwa sababu nyingine.
14 Ndugu wanaostahili hupewa mgawo wa kuwa wakaribishaji wakati wa mikutano katika Jumba la Ufalme. Wanapaswa kuwa chonjo, wenye urafiki na utambuzi. Majukumu yao yanatia ndani kuwasalimu na kuwakaribisha wapya, kuwaonyesha waliochelewa mahali
-