-
Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mipango kwa ajili ya mikusanyiko mikubwa hata zaidi katika Poland ilikuwa inaendelea, mnamo Mei 12, 1989, serikali ilipotoa utambulisho wa kisheria kwa Mashahidi wa Yehova kuwa shirika la kidini. Katika muda wa miezi mitatu, mikusanyiko mitatu ya kimataifa ilikuwa ikiendelea—katika Chorzów, Poznan, na Warsaw—kukiwa na jumla ya hudhurio la 166,518. Kwa kustaajabisha, maelfu ya Mashahidi kutoka zile nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti (U.S.S.R.) na Chekoslovakia waliweza kupata ruhusa iliyohitajiwa ya kusafiri na walihudhuria. Je, kazi ya kufanya wanafunzi ya Mashahidi wa Yehova ilikuwa inazaa matokeo katika nchi hizo ambako kutoamini kuwako kwa Mungu kulikuwa kumeungwa mkono sana na Serikali kwa miongo ya miaka? Jibu lilikuwa wazi wakati 6,093, kutia na vijana wengi, walipojitoa kwa ajili ya uzamisho wa maji kwenye mikusanyiko hiyo.
Umma ungeweza kuona wazi sana kwamba Mashahidi walikuwa tofauti—kwa njia yenye kufaa sana. Kwenye magazeti ya umma, walisoma taarifa kama zile zifuatazo: “Wale wanaoabudu Yehova Mungu—kama vile wanavyosema wenyewe—huthamini sana vikusanyiko vyao, ambavyo kwa kweli ni udhihirisho wa umoja miongoni mwao. . . . Kuhusu utaratibu, hali ya amani, na usafi, washiriki wa mkusanyiko ni mifano ya kuigwa.” (Życie Warszawy)
-
-
Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 504]
Baadhi ya wanaotaka kubatizwa katika Chorzów, Poland, katika 1989
-